Bastola ya Dito yapotea kiaina

34 views
Skip to first unread message

Aik

unread,
Nov 8, 2006, 11:24:12 AM11/8/06
to Kilimanjaro Forum
Ile bastola inayodaiwa kutumiwa katika mauaji ya dereva wa daladala
Hassan Mbonde na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Kapten Mstaafu
Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, imeyeyuka na hadi sasa Polisi wanaumiza
vichwa katika kuinasa.

Bastola hiyo ambayo bado inaendelea kusakwa, inadaiwa kupotea wakati wa
purukushani zilizofanyika mara baada ya tukio hilo la kuuawa kwa dereva
wa daladala pale kwenye makutano ya barabara za Bagamoyo na ile ya
kuelekea Kawe.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Dito ameieleza polisi kuwa silaha hiyo
ilipotea muda mfupi baada ya tukio ambapo kundi la watu lilimvamia na
kumfanyia vurugu iliyosababisha upotevu wa bastola hiyo.

Kufuatia kuyeyuka huko kwa bastola, polisi hivi sasa ingali ikiendelea
na msako kabambe wa kuitia mikononi.

Aik

unread,
Nov 8, 2006, 11:25:24 AM11/8/06
to Kilimanjaro Forum
Don't be suprised if this man walks out easily.

Mariam

unread,
Nov 8, 2006, 12:52:36 PM11/8/06
to Kilimanjaro Forum
Ditopile ajiuzulu ukuu wa mkoa
http://www.darhotwire.com/dar/Habari/2006/11/08/25938.html

"Hivyo napenda kukuarifu kuwa nimekubali ombi lako la kujiuzulu wadhifa
wa Mkuu wa Mkoa. Kwa mara nyingine tena pole kwa yote. Usiache
kumshukuru na kumuomba Mungu."

Hayoni maneno ya Rais Jakaya Kikwete akikubali kujiuzulu kwa Mkuu wa
Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile-Mzuzuri, anayekabiliwa na kesi ya
mauaji ya raia mjini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu mjini Dodoma
jana usiku, Rais Kikwete amekubali ombi hilo kufuatia barua
aliyoandikiwa na Ditopile Jumapili iliyopita, siku moja kabla ya
kufikishwa mahakamani, akimuomba Rais akubali kujiuzulu kwake.

Rais alieleza: "kuomba kwako kujiuzulu wadhifa wako wa Mkuu wa Mkoa ni
uamuzi wa busara na hekima. Unatoa fursa kwa taratibu stahiki za
kisheria kufanyika bila ya vizuizi visivyokuwa vya lazima. Ni heshima
kwa taifa letu linalozingatia utawala wa sheria.

Wajuzi wa mambo wanadai Braza Dito ilikuwa lazima aachie ngazi tu, hata
kama asingetangaza kujiuzulu kulingana na kosa linalomkabili lazima
angevuliwa cheo hicho.

filla...@yahoo.com

unread,
Nov 9, 2006, 11:20:51 AM11/9/06
to Kilimanjaro Forum
I would predict he might walk easily simply by having strong lawyers
who knows how to create doubts and issues in a case.I suspect the
victim family have no powerful lawyer in their side.If i recall in some
of the early news they said Ditopile is suffering from medical
complications etc.So that is a good start in his side.Even if he is
convicted the doctor might argue to get the out sentence or
otherwise.But that is my prediction let wait and see.

Aik

unread,
Nov 9, 2006, 2:03:09 PM11/9/06
to Kilimanjaro Forum
>From Issa Michuzi's blog: http://issamichuzi.blogspot.com/

"serikali leo imetembelea familia ya hayati hassan mbonde dereva wa
daladala aliyepigwa risasi na mshukiwa ditopile mzuzuri, na kutoa pole
kwa wafiwa na ubani wa 500,000/- . hapo ni katibu mkuu kiongozi mh.
philemon luhanjo akikabidhi ubani kwa baba mzazi wa marehemu mh. mzee
mbonde huko kawe. jk pia katuma salamu za rambirambi na inatarajiwa
atakwenda kuhani pindi arudipo safari, meibii jumapili hivi. mh. mzee
mbonde amemwambia mh. luhanjo kwamba hayati hassan ndo lilikuwa tegemeo
la familia, na kuondoka kwake ni pigo kubwa kwao"

K-Forum

unread,
Nov 17, 2006, 12:00:40 PM11/17/06
to Kilimanjaro Forum
THIS ARTICLE HAS BEEN MOVED TO www.kforumonline.com AND WILL SOON BE
BLOCKED AND REMOVED. PLEASE CONTINUE ALL DISCUSSIONS/ RESPONSES IN THE
NEW SITE.
THANK YOU.
K-FORUM
________________

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages