Mawazo ya
vijana wengi leo yanaamini kuwa, umasikini ni
mzigo mkubwa usiokuwa na ufumbuzi.
Kitaalamu mtu anapokuwa na mawazo ya
kutokufanikiwa hawezi kufanikiwa kwa sababu
mafanikio huhitaji nguvu na nguvu za mwili
haziwezi kujitokeza kama hazikuvutwa
kufanya kazi. Kwa msingi huo, ili mtu aweze
kufanikiwa lazima mawazo yake yakubali
kuwa mafanikio ni sehemu ya lazima katika
maisha. Jambo hili haliwezi kutokea mpaka
kijana mwenyewe aliyelelewa kwenye mawazo
ya kushindwa apigane vita na mawazo ya
kutofanikiwa na kuyashinda.
Like fb page yetu inaitwa>MAKI INSPIRE
BLOG>makinspire.blogspot.com
mr motivation