Nifikishieni hii barua kwa BABA wa TAIFA
Dear Mwalimu,
Salaamu
Tangu uondoke, hali hapa Tanzania imebadilika sana. Siku hizi Mlima Kilimanjaro uko Kenya,
Ziwa Nyasa liko Malawi,
Tanzanite inatokea Kenya na Afrika ya Kusini,
TANESCO nasikia ni ya Lowassa,na kiwanda cha nguzo mufundi kipo Sauzi Africa!
Sheikh Ponda ndiyo IGP wa Tanzania na kwa Zanzibar ni Sheikh Farid japo si wateule wa rais ambaye
naye (rais) amehamishia makao yake uwanja wa ndege
Mwalimu Tangu uondoke historia ya nchi na jiografia yake vinachukua sura nyingine,
kwa sababu siku hizi Tanzania imetokana na visiwa vya Zimbabwe na Pemba.
Kuna tetesi kuwa hata kaburi lako Mwalimu halipo Tanzania na mbaya zaidi hata ile kauli mbio yako kupambana na UJINGA, MALAZI NA UMASIKINI sasa wameongeza adui mwingine UFISADI ndiyo ametawala!
Wasalimie wote huko uliko.
Mtiifu,