Udaku Specially

169 views
Skip to first unread message

Udaku Specially

unread,
Nov 18, 2014, 4:14:20 PM11/18/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Wema Sepetu Akubali Matokeo ya Kuachana na Diamond..Soma Ujumbe Alioandika

Posted: 18 Nov 2014 10:25 AM PST

This is what she wrote on her instagram page:

'Wen one door closes, dont stress..!, dont think...!God has another one with a Brighter and Nicer future jus around da corner waiting for u to Open IT...!!! Take it from ME...!!!'

Imegundulika Kumbe Mastaa wa Kike Bongo Hujiuza Kupitia Mitandao ya Kijamii

Posted: 17 Nov 2014 10:32 PM PST

MWANADADA mwenye umbo la utata Bongo, Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’ ameibuka na kueleza kwamba mastaa wamegundua njia mpya ya kujiuza ambayo ni kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.

Akistorisha na gazeti hili, Aunt Lulu alisema mastaa wengi wa kike wanajiuza kwenye mitandao ambapo mapedeshee waliopo mikoa mbalimbali wakishaziona picha zao huwa wanawatafuta kwa udi na uvumba ambapo wanawapigia simu na kuwatumia fedha na tiketi za ndege ya kwenda na kurudi.

“Yaani mastaa wa kike hatulali unakuta pedeshee anakutumia tiketi ya ndege unamfuata mkoani ukienda usiku asubuhi umesharudi Dar unaendelea na mambo yako ndiyo maana unawaona wasanii wengi wa kike wana fedha lakini kazi wanazozifanya huzioni,” alisema Aunt Lulu.
GPL

Pombe si Chai, Binti wa Kiarabu Amwaga Radhi Hadharani.. Midume Yatoka Udenda

Posted: 17 Nov 2014 10:28 PM PST

POMBE si chai! Binti mrembo mwenye asili ya Kiarabu ambaye jina halikupatikana mara moja, amejikuta akifanya vioja baada ya kulewa chakari na kusababisha midume kumtolea udenda, Ijumaa Wikienda lilimpiga chabo.

Tukio hilo la aibu lilijiri kwenye onesho la Kundi la Mashauzi Classic ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar ambapo lilikuwa likitambulisha albam yake mpya ya Sura Surambi, Sura Siyo Roho.

Awali binti huyo alionekana ukumbini humo akiwa mpole na mwenye sura ya soni huku akipata kilaji polepole kabla ya kumkolea na kuwa staa wa kubinuka kihasarahasara na kumwaga ‘lazi’ mbele ya kadamnasi huku akiacha sehemu ya maungo yake nyeti kweupe.

“Jamani pombe mwanaharamu. Muone yule binti wa Kiarabu, kaja mpole lakini hebu ona vituko utadhani kuna skruu imefunguka kichwani,” alisema mmoja wa mashuhuda.Katika hali iliyoonekana kuzidi kuelemewa na kilaji, binti huyo alianza kuwavaa wanamuziki stejini na kuwakumbatia kisha kuinua mguu na kurusha mateke ya kinyumenyume kama mwanasoka, Cristino Ronaldo wa Real Madrid.

Vioja vya binti huyo havikuishia hapo kwani aliwavaa wanaume na kuwakatikia vilivyo.
Wakati tukio hilo likiendelea, jamaa mmoja alimfuata akidai ni mkewe ambapo alimfokea mwanahabari wetu akimtisha kwamba endapo akiziona picha gazetini atamfanya lolote akafie jela Segerea.

GPL

Tickets za The All White Party Zinapatikana Sehemu Hizi

Posted: 17 Nov 2014 10:12 PM PST

Kiingilio ni VIP Tsh. 20,000 na 10,000 Tikets kuanzia leo zinapatikana at:- ..........1. Samaki Samaki Mliman City 2. Samaki Samaki Mjini 3. City Sports Lounge Mjini 4. Clouds Media Mikochen.....VIP tikets zipo chache so wahi.mapema please!.....kuingia ni kwa Tikets tu please usije kuniulizia Mlangoni....kama unanijua sana nitafute sasa kabla.ya Jumamosi lakini PLEASE USIJE KUNITAFUTA MLANGONI......DRESS CODE:- White + Gold + Light Blue......usiku wa kiama U know I loooove it!-Lemutuz

Joyce Kiria Amwagia Sifa Mumewe Asema Anafaa Kuwa Mbunge wa Mwanga 2015

Posted: 17 Nov 2014 10:08 PM PST

'Siku zote Taifa lolote lile linaanzia kwenye ngazi ya Familia... Baba au Mama ndani ya Familia akiwa anawajibika vyema kwa Familia yake ni wazi kwamba Familia husika itakuwa na furaha na Amani pamoja na Maendeleo yenye tija kwa wanafamilia... kadhalika watu hao wakipewa jukumu la kuongoza jamii ni wazi kwamba jamii itafaidika na ule uwajibikaji wao kwa kupata huduma bora na kwa wakati.....

Kwa sababu hiyo na mtazamo huo, Mume wangu Henry Kilewo ni Mume na baba bora katika Familia yetu, anatekeleza majukumu yake kama baba na kama Mume vizuri kabisa... ninaimani wananchi wa Mwanga mkimchagua 2015 kuwa Mbunge wenu hakika hamtajuta....

Kwa sasa yupo jimboni kwake Mwanga katika maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa... anaamini katika kuweka msingi mzuri, yaani timu atakayokuja kushirikiana nayo wakati ukifika, ili ile kazi ya kuwaletea Maendeleo Wana Mwanga iwe rahisi zaidi... Nami ninamuunga mkono Mume wangu kipenzi katika Ndoto yake hiyo ya kuongoza Jimbo la Mwanga kuanzia 2015... All the best my Love Henry...' Joyce Kiria

Msanii Linex Katapeliwa Sh.11 millions, Steve Nyerere Ahusishwa kwa Utapeli

Posted: 17 Nov 2014 09:58 PM PST

Linex msanii wa bongo fleva anaetamba kwa sasa na wimbo wa wema kwa ubaya amedai kutapeliwa shiling 11 milion na jamaa ambaye anaitwa Minyamihela ambaye Steve Nyerere alimuunganisha na Linex na huyo Minyamihela ili aweze kumnunulia gari.

Baada ya kupewa gar Linex alilitumia kwa muda wa siku mbili ndipo huyo Minyamihela kuja kulichukua akimuahid atampatia gari jingine, lakini toka huo mwezi wa kwanza hadi leo Linex hajapewa gari lake na wala jamaa(Minyamihela) hajarudisha hizo pesa na kibaya zaidi jamaa hapokei simu ya Linex. 

Linex anaomba ushauri afanyaje?

Lady Jay Dee 'Niacheni Niishi Maisha yangu Bila Stresi, Mimi Sio Yesu au Bikira Maria

Posted: 17 Nov 2014 09:51 PM PST

Wakati kukiwa na maneno mengi juu ya madai ya kuvunjika kwa ndoa yake na mtangazaji  maarufu Bongo wa Redio E-FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’, supastaa wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo a.k.a Jide au Jaydee amefunguka kuwa naye si mkamilifu kwani siyo Yesu wala Bikira Maria. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, wikiendi iliyopita Jide aliamua kuvunja ukimya kufuatia maswali ya mashabiki wake lukuki waliotaka afunguke kinachoendelea katika maisha yake. “Watu wanategemea niwe kama Yesu au Bikira Maria? Siwezi, mimi ni mwanadamu tu. Hakuna aliye mkamilifu. Niacheni niishi maisha yangu bila stresi. Mwingine yeyote pia aishi maisha yake. Kila mmoja anatakiwa awe huru,” aliandika Jide.

Lundenga Kikaangoni Tena Baada ya Sitti Kushindwa Kurudisha Zawadi Zote Alizopewa

Posted: 17 Nov 2014 09:37 PM PST


Lundenga na Kampuni yake ya Urembo matatani tena baada ya Basata kuhoji kwanini Sitti Mtemvu Bado Hajarudisha zawadi zote alizoshinda Katika Mashindano hayo ya Urembo..
Basata Imesema Sitti inaitajika kurudisha zawadi zote alizoshinda kuanzia Miss Temeke, Miss Changombe na Miss Tanzania 2014 kwa vile huko pote alishiriki huku amedanganya Umri ..
Kazi Ipo .....

Je Unafikiri Hapo Haki Inatendeka Kweli ?

Wanawake Kenya Waandamana Kupinga Kuvuliwa Nguo Hadharani Kwa Wanao Vaa Nguo Fupi

Posted: 17 Nov 2014 09:23 PM PST

Wanawake mjini Nairobi, Kenya leo wameandamana kupinga kitendo cha mwanamke mmoja kuvuliwa nguo wiki jana kwa madai kuwa alikuwa amevalia sketi fupi sana.
Wanawake wengi walikerwa na kitendo hicho wakisema kuwa kila mwanamke ana haki ya kuvalia mavazi yanayomfurahisha.
Hiyo wiki jana kanda ya video ilisambazwa kwa mitandao ya kijamii ikionyesha mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina hadi sasa akivuliwa nguo zake na wanaume katika kituo cha magari ya abiria kati kati mwa Nairobi.

Wanawake mashuhuri wakiwemo wasanii, wanasiasa na wanaharakati walilaani kitendo hicho wakihoji kwani mavazi ya mwanamke yanamhusu nini mwanamume ambaye sio mumewe wala jamaa yake.
Baadhi walikitaja kitendo hicho kuwa cha kinyama na kinachokiuka haki za wanawake.
Msanii mmoja mashuhuri Nyota Ndogo alinukuliwa akisema ikiwa wanaume wanawavua nguo wanawake kwa kile wanachosema ni mavazi yasiyo ya kiheshima, basi na wanaume wanaolegeza long'i zao na wao basi pia wavuliwe nguzo zao.

Mama Yangu Amenionyesha Baba Yangu Halisi Baada ya Miaka 38, Nimemkataa Laivu

Posted: 17 Nov 2014 08:54 PM PST

Mimi nina miaka 38 sasa, msomi wa elimu ya juu na nina kazi nzuri pia, nilikuwa naishi vizuri na wazazi wangu wawili I mean baba na mama, sasa hapa juzi baada ya ugomvi, mama ameondoka nyumbani na kuniambia eti baba nilienae sio baba yangu biological na baada ya kikao kirefu nimeonyeshwa baba mwingine wanaomsema ndio baba biological ila mbele ya watu wote nilimkana na kumwambia asinijue kabisa na wala sitaki kuharibiwa maisha yangu. 

Mimi nina baba yangu ambae amenilea na ndio naamini ni baba halisi kwangu, sasa wanakazania DNA mimi nikasema sitaki chochote na nisiingizwe kwenye ugomvi wa wazazi wangu na ninampenda sana baba yangu alienilea kwasababu amenisomesha shule za gharama na amenitembeza duniani na kunipa kila nilichotaka mpaka hapa nilipo namwona kama mtu namba moja muhimu kwangu hapa duniani.

Je waungwana nilichofanya ni makosa?

Ripoti Maalumu ya CAG Kuhusu Akaunti ya Escrow Yakabidhiwa kwa Mwenyekiti wa Pac Zitto Kabwe

Posted: 17 Nov 2014 08:47 PM PST

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai akikabidhi Ripoti maalumu ya CAG Kuhusu akaunti ya ESCROW kwa Mwenyekiti…

Tujikumbushe:

Ripoti ya sakata la uchotaji wa Dola za Marekani 200 milioni katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyotua bungeni wiki iliyopita, imeibua mambo mazito baada ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kugundua kuwa fedha zilizochotwa kwenye akaunti hiyo zilikuwa mali ya Tanesco.

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinaeleza kuwa fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo ni Sh306 bilioni wakati madai ya Tanesco kwa IPTL ni Sh321 bilioni, hivyo fedha zote za Escrow zilipaswa kwenda Tanesco na bado ingekuwa inadai.

Ukaguzi wa akaunti hiyo uliamuliwa na Serikali baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila kudai kuna ufisadi katika uchotaji wa fedha hizo katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akaunti hiyo ilifunguliwa baada ya kutokea mgogoro wa kibiashara baina ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Kampuni ya kufua umeme ya IPTL.

Hatimaye Kivuko Kipya cha Safari za Dar es Salaam Kwenda Bagamayo Chawasili

Posted: 17 Nov 2014 08:42 PM PST


Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli leo amepokea kivuko kipya cha MV Dar es Salaam chenye uwezo wa kubeba abiria 306.

Kivuko hiki kipya kitatoa huduma ya usafiri kati ya Jiji la Dar es Salaam na mwambao wa Bahari ya Hindi hadi Bagamoyo. Kivuko cha MV Dar es Salaam kitakuwa na kasi kuliko kivuko chochote Afrika ya Mashariki na hasa mwambao wa bahari ya Hindi ukiacha Afrika ya Kusini.

Itakumbukwa waziri Magufuli amekuwa akiahidi kufanya jitihada za kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kununua kivuko kitakachofanya safari zake katika mwambao wa bahari ya Hindi mpaka Bagamoyo.

Kivuko hiki mkombozi wa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kimejengwa na kampuni kutoka Denmark kwa gharama ya shilingi (Tanzania) bilioni 7.9.

Sifa kubwa ya kivuko cha MV DAR ES SALAAM:

1. Kina uwezo wa kubeba abiria kati ya 306 waliokaa hadi 400,

2. Kina spidi (speed) kubwa kuliko vivuko vyote Tanzania na hata Afrika ya Mashariki

3. Kina ghorofa mbili (Two Floors)

4. Kwa ndani kina makochi mazuri kabisa ya kisasa ikiwa pmoja na life jacket

5.Kina tekinorojia ya kisasa kabisa ya Nivigation.

Mtoto Mwingine Atekwa, Auawa na Kukatwa Nyeti

Posted: 17 Nov 2014 08:34 PM PST

WIMBI la utekaji na mauaji ya watoto katika Jiji la Dar bado ni tishio kufuatia wiki iliyopita, maiti ya mtoto Nuru Mohamed (7) mkazi wa Majohe Kichangani Wilaya ya Ilala, kuokotwa ikiwa imeharibika vibaya, tena baadhi ya viungo vyake vikiwa vimenyofolewa.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Novemba 6, mwaka huu, majira ya saa 12 jioni, baada ya watoto wenzake aliokuwa akicheza nao kudai kuwa Nuru alichukuliwa na mtu aliyekuwa amevalia mavazi ya Kininja na kutokomea naye.

Baadhi ya mashuhuda waliokuwa eneo la tukio, walisema mwili wa mtoto huyo ulikutwa ukiwa hauna sehemu za siri, matiti, nyama ya kisogoni na makalio kukatwa na kuzibwa na gundi hali iliyoashiria ushirikina.

BABA MZAZI PICHANI ASIMULIA ILIVYOKUWA
“Nakumbuka siku ya kutoweka kwake, nilikua kazini nikapigiwa simu saa 12.45 jioni na kuelezwa Nuru ametekwa na mtu aliyevaa kininja, aliyemrubuni kwenda kumnunulia biskuti. “Nilielezwa kwamba muda mfupi baada ya kutoweka, watoto wenzake walipatwa na hofu na kumwambia mama yake kwamba kuna mtu kaondoka na marehemu hali iliyomfanya kuinuka na kuanza kufuatilia bila mafanikio.

“Niliungana na mke wangu pamoja na ndugu wengine kumtafuta hadi asubuhi bila mafanikio, nikiwa nipo maeneo ya Chamazi saa 2 asubuhi nilipigiwa simu na kuambiwa mwili wa mwanangu umepatikana maeneo ya lwa Mkandawile ukiwa umeharibika, nilienda na kukuta kuwa ni yeye.

“Tulitoa taarifa polisi ambao walifika eneo la tukio na kuuchukua mwili hadi Hospitali ya Amana na muda mfupi baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari tuliuchukua na kuuzika makaburi yaliyopo maeneo ya ninakoishi,” alisema

Mjunbe wa Shina namba 15 Tawi la Majohe, Matanzira Thomas maarufu kwa jina la Kobra alisema kwamba matukio hayo ya utekaji watoto, kuwaua na kuondoka na sehemu ya viungo ni hatari hasa katika nchi ya amani kama Tanzania, hivyo ameliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini na kuwakamata watu hao hatari.

Download Wimbo Mpya Kutoka Kwa Mwasiti Akimshirikisha Kingzilla. Wimbo Unaitwa Leo.

Posted: 17 Nov 2014 08:30 PM PST

Download Wimbo Mpya Kutoka Kwa Mwasiti Akimshirikisha Kingzilla. Wimbo Unaitwa Leo.
You are subscribed to email updates from Udaku Specially
To stop receiving these emails, you may unsubscribe now.
Email delivery powered by Google
Google Inc., 1600 Amphitheatre Parkway, Mountain View, CA 94043, United States

Udaku Specially

unread,
Nov 19, 2014, 4:50:00 PM11/19/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Dully Sykes na Maunda Zorro Watoa Wimbo wa Matusi Mwanzo Mwisho..Download Hapa

Posted: 19 Nov 2014 07:04 AM PST

Dully Sykes na Maunda Zoro Wameachia Wimbo wenye Mahadhi ya Matusi Ambapo Dully anasikika akiimba mambo ya chumbani huku Maunda Zorro Akilia kwa Mahaba..
Unaweza Kuudownload wimbo huo Hapa chini usikie mwenyewe...

Mchepuko wa Zari The Boss Lady (Farouque) Abwaga Manyanga na Kusema Haya

Posted: 19 Nov 2014 06:42 AM PST

Ninaripoti kutoka Uganda kama ifuatavyo: 

Baada ya Diamond kujisevia Zari kiulaini bila kutumia nguvu boyfriend wa Zari aamua kujiweka kando kwa madai kwamba ni bora awe single kuliko kuwa na Mwanamke asiyejiheshimu. Ameorodhesha tuhuma 5 ikiwemo kupasha kiporo na baba watoto wake, kuwa na mitafaruku ya mara kwa mara kuhusu mali za exhusband Ivan, kukutana na Diamond kwenye Ndege kisha kumalizana kiutu uzima na nyingine 3 Kama alivyoziorodhesha. 


Hata hivyo mchepuko mwingine wa Zari (basketballer LK4 BBA season 7 ambaye alikuwa anachepuka na Zari wakati Zari yuko ndoani) alimlaumu farouque kwa kumuuliza "are you mad"? 


Pamoja na lawama za LK4 bado jamaa anaonekana kuchoshwa na uchepukaji wa bidada kwani genye zake ziko karibu. 


Farouk Sempala is hurting following cozy pics of his ex-lover Zari and Tanzania's Diamond Platnumz that went viral. Diamond Platnumz and Zari at a Beach in Dar. Using his facebook profile, he made this post;

"I would rather remain single than have a beautiful wife that does not respect herself and turns out to justify her wrongs as rights, it's just a waste of time and calories." The post was followed by five other points and one of them was tagged to Zari and Diamond Platnumz - You bump into a singer on a plane and you call that a project!

Mwanamke Aliye mnyoa Nywele Kwa Kisu Mwanamke Mwenzake Arusha Yamkuta Makubwa..

Posted: 19 Nov 2014 06:10 AM PST

Haya jamani majibu si mnakumbuka haya dada alimuabisha mwanamke mwenzie hatimae sasa mwanaume huyooo kamchukua kimada chezea wanaume wewe...



Sakata la Tegeta Escrow Lilivyoanza Mpaka watu Kuitana Tumbili na Mwizi

Posted: 19 Nov 2014 02:12 AM PST

Kashfa ya Tegeta Escrow iliibuliwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila.Kuibuliwa kwa kashfa hiyo, kulisababisha Kafulila kuingia kwenye malumbano makali yaliyowafikisha katika kutoleana maneno ya dharau na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, bungeni.

Maneno hayo ya dharau yalihusisha Jaji Werema kumwita Kafulila kuwa ni tumbili na Kafulila kumwita Jaji Werema mwizi.Baadhi ya wabunge wamekuwa wakishinikiza wakitaka ripoti hiyo pamoja na ile ya uchunguzi uliofanyw a na Takukuru ziwasilishwe bungeni ili zikajadiliwe na wabunge ili ukweli ujulikane.

Tayari nchi wahisani zimetangaza kuikatia misaada serikali ya zaidi ya Sh. trilioni 1 kutokana na kashfa hiyo.Akaunti ya Tegeta Escrow ilifunguliwa kutokana na kutoelewana kuhusu gharama halisi na halali za umeme unaozalishwa na kampuni ya kufua umeme ya IPTL na kuuzwa Tanesco.

Mahakama ya Usuluhishi ya Kimataifa (ICSID), katika uamuzi wake wa Februari 2014, ilitoa hukumu kuonyesha kwamba Tanesco walitozwa
kiwango cha juu zaidi ya kilichopaswa kulipwa kwa IPTL.

Kwa uamuzi huo, ni dhahiri kwamba fedha zilizokuwa zimehifadhiwa kwenye akaunti ya Escrow zilipaswa kugawanywa kwa IPTL na Tanesco baada ya hesabu kufanyiwa marekebisho upya kwa viwango halali, lakini badala yake fedha hizo zilitoweka ghafla kwenye akaunti hiyo.

KILICHOMO KATIKA RIPOTI YA CAG
Matokeo ya ukaguzi uliofanywa na CAG kuhusiana na kuchotwa kwa Sh. bilioni 306 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow yameiweka matatani Ofisi ya Mwananasheria Mkuu wa Serikali (AG), huku yakizitambua fedha hizo kuwa ni za umma.

Vyanzo vyetu mbalimbali vimebainisha kuwa Ofisi ya AG inadaiwa kuingia matatani, baada ya ripoti ya ukaguzi huo iliyovuja, kubaini kwamba, inahusika moja kwa moja katika kuisababishia serikali hasara ya jumla ya Sh. bilioni 321 katika kashfa hiyo.

Pia Wizara ya Nishati na Madini, nayo pia inatajwa na ripoti hiyo kuhusika katika kuisababishia serikali hasara hiyo.

Vilevile, Bodi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) nayo pia imeingia matatani, baada ya kuhusishwa na ripoti hiyo kwa tuhuma za kulikosesha shirika hilo kiasi hicho cha fedha.

Ofisi ya AG inahusishwa na kashfa hiyo, baada ya ripoti hiyo kueleza kuwa ilivunja sheria makusudi kwa kuelekeza kuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye gharama za uendeshaji (capacity charges), ambazo Tanesco walilipishwa na IPTL, isilipwe.

Maelekezo hayo ya ofisi ya AG yanadaiwa kusababisha serikali kupoteza mapato ya Sh. bilioni 21.

Moja ya Sababu ya Kenya kuwa Juu ya Tanzania Kiuchumi

Posted: 19 Nov 2014 01:55 AM PST

Leo katika taarifa ya habari saa 1 jioni ya kituo cha televisheni cha K24 cha Kenya imeonesha mchakato wa usajili na uandikaji namba mpya za magari nchini humo, uandishi wa vibao vya namba za magari unaofanywa na wafungwa wa gereza nchini humo.

Uandishi wa vibao vya namba za magari ni mradi endelevu tena wenye kuingiza fedha nyingi mno. Kwa hapa kwetu,mradi mara ya kwanza ilipewa kampuni binafsi. Inasemekana kampuni hiyo ina ubia na Waziri Mkuu wa zamani,ambaye ni fisadi mjanja sana. Ameificha miradi yake ya kifisadi kwenye majina na makampuni yaliyochini ya watu tofauti tofauti.

Hapa nchini,makampuni yenye kuzaa faida yamechukuliwa na viongozi mafisadi,mfano,makampuni ya mawasiliano yalichotwa hisa za umma kupewa wageni kwa niaba ya mafisadi wazawa walio ndani ya Serekali, angalia TTCL,ATCL, aidha, inasemekana tiGO ilipokuwa chini ya MIC ltd serikali ilikuwa na hisa % 17 ambazo zilichotwa kinamna na spika mmoja wa zamani wa bunge la JMT.

Huko Kenya kampuni ya simu ya umma ndiyo inashikilia na kutamba katika nyanja ya mawasiliano nchini humo.

Kwa mfumo huu, Kenya itendelea kututimulia vumbi.

Hali yazidi Kuwa Tete Escrow, Hapatoshi Dodoma

Posted: 19 Nov 2014 01:42 AM PST

IKIWA ni siku chache tu baada ya kutolewa kwa taarifa za kukabidhiwa kwa ripoti ya ukaguzi wa akaunti ya ESCROW, uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), kwa spika na kamati ya mahesabu ya serikali PAC, mengi yameibuka.


Hali hiyo inatokana na kuwepo kwa mgawanyiko wa wabunge kuhusu na jambo hilo huku kila upande ukiwa na mtazamo wake tofauti juu ya jambo hilo, ambalo wabunge wengi wanaamini linapikwa na halizungumzwi ukweli.


Taarifa kutoka Dodoma zinasema kwamba wabunge wengi wameshitushwa na kuvuja kwa taarifa kuwa kamati ya PAC imelivalia njuga suala hilo, baada ya kushindwana kuafikiana mgao wa malipo kutoka kwa wamiliki wa kampuni ya IPTL/PAP ili kulizuia kulimaliza katika Kamati lisifike bungeni mapema mwaka huu.


Taarifa hizo zinasema kamati ya PAC iliwatumia mwanasheria aliyefahamika kwa jina la Albert Msando ambaye ni msaidizi wa kisheria wa Zitto Kabwe na Beatus Malima kujadili juu ya malipo watakayolipwa PAC ili kuidhibiti ripoti hiyo na namna ambavyo PAC ingetoa hukumu ya awali.

Vithibitisho ambavyo baadhi ya waandishi wameonyeshwa na baadhi ya wabunge hao, vinaonyesha mijadala iliyokuwa ikiendelea bungeni kuwa mingi ni ya kupikwa na ya kimkakati inayotokana na hasira za kutokupatiwa malipo waliyoomba PAP na hivyo kulitaka bunge lipigie mhuri kitu ambacho ni mgogoro unaotawali na maslahi binafsi.


Haijafahamika mara moja kwamba ni kiasi gani kimeombwa na kamati ya PAC kwa PAP ili walifunge jambo hilo, mlakini baadhi ya wabunge hao wamesema wapo tayari kuweka wazi kila kitu ili kila mtu avune alichopanda.


‘’Ni kweli kila mtu atavuna alichopanda, kama wanataka kutugeuza wabunge wote ni ‘Rubber stamp’ tuhalalishe hukumu inayotokana na hasira zao za kunyimwa mgao, basi wamegonga mwamba’’. 
Alisema mmoja wa wabunge hao anayetokea chama kimoja cha upinzani akijibu kauli ya Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe aliyenukuliwa na gazeti moja hivi karibuni.


Hivi karibuni Filikunjombe, alisema katika gazeti hilo, kwamba kila mtu atavuna alichopanda katika sakata hilo, baada ya kupokea ripoti ya CAG kutoka kwa Naibu Spika, Job Ndugai.

Akizungumza kwa kujiamini, mbunge mwingine ambaye pia ameomba ahifadhiwe jina lake kwa sasa anasema ’’Hata Kamati yenyewe ya PAC imegawanyika vipande vipande, wakubwa wao wamevuta mzigo wa kutosha na wenzao wanawaburuza, halafu kazi nzima ya kamati inapelekeshwa kutoa sifa kwa watu wawili tu ambao ni Zitto na Filikunjombe, huu ni upuuzi’’.


Mbunge huyo alisema sisi sote ni wanasiasa, unafikiri nani atakuwa tayari kufanya kazi, halafu sifa ziwaendee watu wawili tu kwamba wao ndio wanaakili sana na wana uchungu sana na nchi.
‘’Hebu jiulize kamati ina wajumbe zaidi ya 20 lakini kila kitu zitto na deo wanajiweka kimbelembele, sasa na safari hii wanapoumbuliwa kwa madili yao ya rushwa wakae kimbelembele hivyo hivyo’’. Alisema mbunge huyo.


Hata hivyo, taarifa kutoka kwenye ripoti iliyovuja ya CAG haionyeshi kwamba kuna tatizo kwenye ukaguzi walioufanya wa akaunti ya ESCROW, badala yake umeibua madai mapya ambayo sio msingi wa uchunguzi walioagizwa kufanya.


Itakakumbukwa kwamba akaunti ya ESCROW ilifunguliwa rasmi Julai, 5 2006, wakati ripoti ya CAG inaonyesha mapungufu ya kuanzia Januar 2002 mpaka Desemba 2006 huku ripoti yenyewe ilipaswa kujikita kati ya 2006 mpaka 2013 ilipofungwa.


‘’Hatupaswi kuwaadhibu watu kwa sababu tu tunawachukia, au kwa sababu tunachuki na tofauti nao binafsi ama za kisiasa, sisi kama bunge ni lazima tufanye kazi zetu kwa kudhibiti hisia zetu, wanachokifanya kina Zitto, David Kafulila na Deo, ni chuki binafsi na si uzalendo kama wanavyotaka iwe, kama ni wazalendo wasingefanya kama haya wanayofanya’’. alisema mbunge huyo.


Alisema mbunge huyo, wabunge hao baada ya kuona ripoti ya CAG haiwatii hatiani serikali na wanaowachukia wao, wanalazimisha kusema kuwa kuna hasara ya bilioni 321. Waache kuwafanya wabunge watoto wadogo kwa kuwa kila kitu tunakijua.


Wakati hayo yakiendelea, jana asubuhi Mbunge wa Mtera-CCM, Livingstone Lusinde aliiomba mwongozo kwa Naibu Spika, Job Ndugai kuhusiana na kubana kwa ratiba katika suala la akaunti ya ESCROW huku jambo hilo likiwa na hamasa kubwa kwa watanzania.
“Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Kamati ya Uongozi ya Bunge iongeze siku au muda katika kujadili suala hili, kwa kuwa ni jambo kubwa linalohitaji kujadiliwa zaidi, tuna mengi tunayoyajua, makando kando ya wanaotuhumiwa na wanaotuhumu pia, kwa kuwa waswahili wana msemo mmoja ukimuona anayelia sana ujue ndio mchawi mwenyewe,’’alisema.


Alisema wabunge wanaolia sana kuhusiana na jambo hilo, wenyewe wana makando makando katika suala hilo kutokana na kuhusika kwa namna moja au nyingine katika sakata hilo, ambalo anaamini kujadiliwa kwa muda mrefu zaidi ndio jambo litakaloweka haki kwa kila mtu.
Hivyo, aliiomba Bunge iongeze siku zaidi kujaidli suala hilo, ambapo Naibu Spika Ndugai alisema atawasiliana na Kamati ya Uongozi ya bunge kuhusiana na mwongozo huo wa Lusinde ili ufanyiwe kazi kwa kuwa jambo hilo lina umuhimu mkubwa kwa taifa.

Chameleone 'Diamond ni Msanii Mchanga Siwezi Kamwe Kumuomba Collabo'

Posted: 19 Nov 2014 01:29 AM PST

Chameleone amesema kuwa application ya Mziiki ambayo Diamond ni balozi wake wa Tanzania ipo kwenye mazungumzo naye ili kumfanya balozi wake wa Uganda na hivyo ilimuomba afanye wimbo na Diamond kama anthem ya Afrika Mashariki.“Lakini we talked about business na hatujamalizana nao. Lakini sio eti mimi nimempigia (Diamond) kumuomba tufanye collabo na kitu kama hicho,” amesema Chameleone. “Wale wa Mziiki app ndo wanahitaji mimi na yeye tufanye kazi ya anthem ya Mziiki app. Wanajaribu kuunganisha yeye na mimi tufanye collaboration lakini sio eti mimi nimemu whatsapp na nimemuomba collaboration , that’s not right,” amesisitiza hitmaker huyo wa Valu Valu.

Am not at a level of asking for a collaboration from any artist in that manner. Sio kwamba sina heshima yake (Diamond) au kitu kama hicho lakini that’s not the truth, haiwezi kuwa hivyo. I have been doing music for the past 14 years, right? So I am not an upcoming artist.

Ali Kiba Kumbuka Majivuno na Maringo Ndivyo Vilivyokupoteza

Posted: 18 Nov 2014 10:23 PM PST

Kwako
staa uliyerudi kivingine na wimbo wa Mwana, Ali Kiba. Vipi uko poa? Bila shaka u-mzima wa afya na unaendelea na harakati zako za kimuziki.Ukitaka kujua hali yangu, mimi ni mzima wa afya namshukuru Mungu maisha yanasonga. Naendelea na majukumu ya kila siku likiwemo hili la kukuandikia barua.

Pasipo kupepesa macho, pamoja na salamu, dhumuni la kukuandikia barua hii ni kwamba kuna kitu kimenigusa nataka kukukumbusha maana akili ya mwanadamu siku zote imeumbwa kusahau.

Ni rahisi sana mtu kula msoto mkubwa lakini ndani ya dakika chache tu pale unapopata mafanikio, unasahau.Nakumbuka kabla ya kuachia nyimbo za Kimasomaso na Mwana ambazo zinaendelea kufanya vizuri hadi sasa, ulikuwa kimya. Najua unaweza usikubaliane na mimi lakini ukimya ule ulitokana na kujisahau baada ya kuwa na mafanikio makubwa.

Kipindi kile ulifanikiwa kuiteka Bongo, kila mmoja alikuwa akikutambua wewe kama namba moja hususan pale ulipofanikiwa kuwa msanii pekee kutoka Tanzania na kwenda kufanya kolabo maalum iliyoandaliwa na legendary wa muziki kutoka Marekani, R. Kelly.

Kiba ulikuwa Kiba kweli. Kipindi hicho ukitaja Diamond, kila mtu anakuuliza ndiyo nani. Hakuna aliyemjua. Kila mmoja alikujua wewe kwamba ndiyo kioo cha Tanzania katika anga za kimataifa, uwezo wako uliheshimika.
Hapo ndipo zilipoanza pozi, majivuno kama siyo maringo. Ukawa unapanga bei yoyote ya shoo hata ya kukomoa ili mradi anayeandaa shoo ashindwe kufanya kazi na wewe.

Pia hapo ndipo ulipokuwa ukitoa ushirikiano hafifu kwa mashabiki wako kwa kujitenga na vyombo vya habari.Ulijisahau ukaona jina ulilolitengeneza linaweza kuendelea kuwepo hata kama usipozungumza lolote kwa mashabiki wako kupitia vyombo vya habari.

Hata hao waandishi waliokuwa wakitaka kufanya mahojiano na wewe kwa faida yako nao ulikuwa ukiwaletea pozi.Mashabiki wakaanza kukumiss katika kazi zako. Wakawa wanakosa habari zako mpya kiasi cha kukuweka kando na kumpa sapoti bwa’mdogo ambaye sasa anakimbiza kinoma, Nasibu Abdul ‘Diamond’ (wakati huo wewe ulimuona wa kawaida sana).

Kaugonjwa ka kujisahau naona tayari kameanza kukunyemelea. Nimetonywa kwamba umeanza tena. Pozi zimeanza, ‘vurugu’ za vyombo vya habari zimeanza kukata.Nahisi zile shoo kadhaa ulizopiga zimeanza kukusahaulisha hata ile mipango yako ya kutoa video za nyimbo zako mpya tena sizisikii. Nikwambie tu, ulipata bahati Watanzania walikupokea kwa mara nyingine maana ipo mifano ya wasanii wengi waliowika wakapotea lakini kila walipotaka kurudi walichemka.

Itumie fursa ya kurudi na kukubalika upya kama fundisho kwako, usikubali kukaa mbali na mashabiki wako. Wape kazi mpya, wape habari zako kila siku ili waendelee kukupa sapoti wasije wakakusahau ukarudi kule ulikokuwa.Kwa leo ni hayo tu, asante kwa kunisoma.

Wasalaam
Erick Evarist

Kinachoendelea Kuhusu Kesi ya Mauaji ya Mwigizaji Lulu Michael

Posted: 18 Nov 2014 10:20 PM PST

Stori: Musa Mateja
KESI ya kuua bila kukusudia inayomkabili mtoto mzuri wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ imewekwa kiporo kufuatia kuwepo kwa kesi nyingi za mauaji mahakamani, Risasi Mchanganyiko limetonywa.

Kwa mujibu wa chanzo makini, kuna uwezekano mkubwa wa kesi hiyo kusikilizwa tena Februari mwakani kutokana na mlolongo mkubwa wa kesi za mauaji zilizopo Mahakama Kuu ya Tanzania.

Chanzo hicho ambacho kipo ndani ya kamati ya majaji wanaoshughulikia kesi hiyo, kimenyetisha kuwa kesi ya Lulu itakuwa ngumu kusikilizwa wakati huu kwani mbali na wingi wa kesi mahakamani hapo, lakini pia majaji na mawakili watakwenda likizo.

“Ujue kesi ya Lulu ilikuwa miongoni mwa ambazo zingesomwa kabla ya mwaka huu kuisha, ila kulingana na vikao vya majaji inaonyesha wazi kabisa mwaka huu itakuwa ngumu hata Januari haitawezekana kwani wana kesi kama tatu za mauaji na baada ya hapo watakwenda likizo sambamba na mawakili kwani nao ndiyo kipindi chao cha likizo,” kilisema chanzo chetu.

Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake, Steven Kanumba, Aprili 7, 2012  maeneo ya Vatican-Sinza jijini Dar.Kifo cha Kanumba kilichotokea nyumbani kwake, kilidaiwa kilitokana na kuangukia sehemu ya nyuma ya kichwa ambapo alipata mtikisiko wa ubongo kisha kuzikwa kwenye Makaburi ya Kinondoni, Dar.
GPL

Makubwa..Kama una Macho Mazima Embu Niambie nini Kinaendelea Hapo Katika Hii Picha

Posted: 18 Nov 2014 10:14 PM PST

Makubwa..Kama una Macho Mazima Embu Niambie nini Kinaendelea Hapo Katika Hii Picha
Wengi Najua Mtakosa..Hahaha

Wakamatwa kwa Kumvua Nguo mwanamke Hadharani Kenya

Posted: 18 Nov 2014 10:12 PM PST

Polisi mjini Nairobi wamewakamata watu 100 katika msako baada ya mwanamke mwingine kuvuliwa nguo katika mtaa wa mabanda wa Kayole mjini Nairobi.
Inadaiwa mwanamke huyo alikuwa amevalia nguo zisizo za heshima.
Naibu kamanda wa polisi mjini Nairobi Moses Ombati, amaenukuliwa akisema wengi wa waliokamatwa walikuwa wanaume walevi.
Bwana Ombati aliongeza kusema kwamba, mwanamke huyo alishambuliwa katika mtaa wa Kayole Jumatatu jioni na kwamba polisi wanaendelea na msako.
Mnamo Jumatatu mamia ya wanawake waliandamana katika barabara za katikati mwa mji kulaani kitendo cha kumvua nguo mwanamke mwingine mapema mwezi huu mjini Nairobi.
Wanawake hao waliandamana kufuatia wito kwenye mitandao ya kijamii chini ya kauli mbiu #MyDressMyChoice yaani vazi langu uamuzi wangu au nitavaa nitakachojiamulia mwenyewe.
Waandamanaji hao wakiwemo wanawake mashuhuri, wanasiasa na wanaharakati waliandamana hadi katika kituo cha mabasi ambako mwanamke wa kwanza alidaiwa kuvuliwa mavazi yake kwa madai alikuwa amevalia 'Mini Skirt'

Rita Sasa Yampeleka Polisi ‘Miss Tanzania’

Posted: 18 Nov 2014 10:00 PM PST

Kashfa ya aliyekuwa Miss Tanzania, Sitti Mtemvu imechukua sura mpya baada ya Wakala wa Uzazi, Vifo na Ufilisi (Rita) kusema kuwa wamekamilisha upekuzi wa taarifa alizotumia kuombea cheti cha kuzaliwa na vielelezo hivyo vimelekwa polisi vikafanyiwe kazi.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, Ofisa mtendaji mkuu wa Rita, Phillip Saliboko na Meneja masoko na mawasiliano, Josephat Kimaro walisema upekuzi wa nyaraka zilizotumiwa na Sitti uliofanywa na wanasheria wao, tayari umekamilika.

“Kazi yetu (Rita) tumeimaliza na upekuzi wa taarifa za Sitti umekamilika na kinachofuata sasa ni kupeleka nyaraka hizo kwenye mamlaka inayohusika ambayo ni polisi, wao ndio wataamua nini cha kufanya,” alisema Kimaro.

Alisema Rita haiwezi kumhukumu moja kwa moja mrembo huyo kuwa alighushi nyaraka na kudanganya ili apate cheti hicho cha kuzaliwa kilichotolewa na Rita Septemba na badala yake wanapeleka vielelezo walivyonavyo polisi ili nao wavifanyie kazi.

“Sisi (Rita) jukumu letu lilikuwa ni upekuzi wa nyaraka, kazi ambayo imefanywa kwa ustadi mkubwa na jopo la wanasheria wetu na hadi sasa imekamilika na kinachofuata ni kuzipeleka nyaraka hizo polisi ambao wao ndiyo wenye jukumu la uchunguzi na kumchukulia hatua Sitti au la,” alisema.

Wakati huohuo, Saliboko akieleza kuwa bado wana changamoto ya baadhi ya watu kudanganya taarifa zao ili wapate vyeti vya kuzaliwa na kusisitiza kuwa wanaandaa mfumo maalumu ili kukomesha udanganyifu huo.

“Tukibaini mtu ametumia udanganyifu ili kupata cheti, kwanza huwa tunamfutia cheti chake na taratibu nyingine za kisheria zinafuata. Tunafanya hivyo kwa watu wote wanaokuja kuomba vyeti kwetu na siyo kwa Miss Tanzania peke yake japo hili la Sitti tunaiachia mamlaka husika ifanye kazi yake,” alisema.

Sitti Mtemvu aliingia kwenye kashfa ya kudanganya umri wake na nyaraka zake mbalimbali zilionyesha alizaliwa 1989, umri ambao umepitiliza ule unaotakiwa kwa mshiriki wa mashindano ya Miss Tanzania, huku cheti chake kikionyesha alizaliwa 1991, hivyo kulazimika kuvua taji hilo.

Wapinzani Wamsulubu Mwakyembe Bungeni

Posted: 18 Nov 2014 09:58 PM PST

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana ilimsulubu Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ikieleza kuwa wizara yake iliingia mkataba wa mradi wa treni za kisasa kutoka Stesheni ya Dar es Salaam hadi Pugu kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) bila kufuata taratibu.

Kambi hiyo ililieleza Bunge kuwa mkataba huo ulisainiwa baina ya mmiliki wa Kampuni ya M/s Shumoja, Robert Shumake na Shirika la Reli Tanzania huku Waziri Mwakyembe akishuhudia.

Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Ofisi ya Waziri Mkuu,  Uwekezaji na Uwezeshaji, Pauline Gekul alitoa madai hayo wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP).

Gekul alisema taratibu hazikufuatwa kwa kuwa haieleweki ni lini Serikali, wakala au Wizara ya Uchukuzi ilitangaza zabuni ya mradi wa treni kutoka Stesheni hadi Pugu kupitia JNIA.

“Pia haijulikani ni lini Serikali ilifanya upembuzi yakinifu kuhusu mradi huo wa reli kwa kufuata taratibu kama zinavyoainishwa na Sheria ya PPP ya mwaka 2010 ambayo inafanyiwa marekebisho hivi sasa,” alisema Gekul na kuongeza: “Haijulikani ni kampuni ngapi ambazo ziliomba tenda ya ukandarasi wa treni na kwamba M/s Shumoja ilishinda tenda hiyo kwa vigezo gani.”

Alisema kwa kifupi ni wazi kuwa Dk Mwakyembe na wizara yake walikiuka vifungu vya Sheria ya PPP. Alivitaja vifungu hivyo kuwa ni 4(1) na (2) vinavyomtaka waziri kutangaza katika Gazeti la Serikali miradi mbalimbali inayotegemewa kufanywa na sekta ya umma kwa ubia na sekta binafsi.

Unapomkamata Mpenzi wako na Mchepuko Nani wa Kum-Face?

Posted: 18 Nov 2014 09:54 PM PST

Inapotokea umemkamata mpenzi wako na mchepuko live nani wa kum-face kati ya mchepuko na mpenzi wako?

Mara nyingi naona asilimia kubwa ya wengi huwa wana attack mchepuko wakisahau mchepukaji ni jitu zima na akili zake ambalo halijawekewa risasi kichwani na kulazimishwa lichepuke.

Nini maoni yako?

Mabibi na Mabwana ile Single Mpya ya Vanessa Mdee na Barnaba Ndio Hii Imetoka

Posted: 18 Nov 2014 09:44 PM PST

Kwanza watu walianza kuitamani baada ya mfululizo wa picha kuendelea kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na imeingia kwenye Top10 ya cover za single mpya Tanzania zilizoongelewa sana.
Barnaba na Vanessa ni marafiki wa muda mrefu lakini hawajawahi kusikika kwenye single moja, ibonyeze brand new hapa chini alafu usiache kutoa maoni yako.

Udaku Specially

unread,
Nov 20, 2014, 4:41:55 PM11/20/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


The All White Party Night 'Tarehe 22/11/2014, Yamoto Band, Fm Academia and Barnaba Watakuwepo at Escape 1

Posted: 20 Nov 2014 08:57 AM PST


Tickets za Jamamosi The All White Party at Escape One sasa zinapatikana qt:- 1. Samaki Samaki Mliman City 2. Clouds FM Mikochen 3. Samaki Samaki at Samora Avenue and 4. City Sports Lounge jengo la Azania Bank karibu na sanamu. Kiingilio 10,000 na VIP 20,000 .....!

Hataki Massage, Romance, Gogo on Bed kwa Ufupi Nimeuziwa Mbuzi Guniani

Posted: 20 Nov 2014 08:18 AM PST

Nimetoka kuoa kabila moja kubwa kaskazini huko hasara tupu kwa kweli
tulikua kwenye uchumba zaidi ya miaka miwili na nusu aliniambia yeye bado bikra kwahiyo nimvumilie hadi ndoa ndo tuta duu nikamkubalia
kweli tumefunga ndoa miezi sita sasa imepita
sijakuta cha bikra wala birika nimeambulia kopo la kufa mtu , pili gogo hajigusi hata kutoa mguno wa uongo kitandani kama nimenunua s3x dolly vile,
hataki kufanyiwa love play , hataki massage kwa ufupi Nimeula
wenye uzoefu hivi atakuja kubadilika? Wadada wa kichaga ndo mlivyo au ananiigizia?

Safari Hii Watuhumiwa wa Wizi wa Mabilioni ya Escrow Kuzikwa Bongo Ama Gate of Heaven?

Posted: 20 Nov 2014 08:09 AM PST

Ni kwa takribani miezi 5 sasa imepita tangu kuibuliwa kwa sakata la ufisadi wa mabilioni ya ESCROW account,kashfa iliyoibuliwa na mbunge wa Kigoma Kusini Davidi Kafulila,kashfa iliyoibua mzozomkubwa bungeni kiasi cha mwanasheria mkuu jaji Fredrick Werema kudaiwa kutoa kauli za kumtishia maisha mh Kafulila ikiwa ni pamoja na kumwita Tumbili,huku akikanusha kwa nguvu zote kwamba fedha hizo za ESCROW zilizotokana na mzozo wa kibiashara kati ya IPTL na TANESCO si za umma bali ni za IPTL na wadau wenzake wa kibiashara.

Sasa kashfa hiyo imeibuka upya na kwa nguvu zote,hasa ikichagizwa na mbinyo wa kibajeti,ambapo nchi wahisani wamegoma kuchangia bajeti yetu ya maendeleo mpaka pale ripoti hiyo itakapowekwa wazi,kinachochangia skendo hiyo kusambaa nchi nzima kama moto wa petrol ni ripoti za mkaguzi na mzibiti mkuu wa serikali na ile ya PCCB ambazo zimekwenda mbali zaidi kwa kutaja kiwango kilichochotwa kwamba ni zaidi y ash Bilioni 320,huku Bohari kuu ya madawa ikiwa haina dawa wala uwezo wa kununua dawa kutokanana kudaiwa zaidi ya bilioni 102

Nikiendelea kukumbuka mwanzoni mwa sakata la EPA, Namkumbuka aliekuwa gavana wa benki kuu Ballali akiumwa gafla na kusafirishwa gafla kwenda nchini Marekani kutibiwa, ambapo hakikupita kipindi kirefu tukatangaziwa kwamba amefariki dunia, ikumbukwe kwamba Ballali ndo aliyekuwa anajua ni nani na nani walichota mabilioni ya EPA; kwa idhini ya nani na kwa matumizi yapi,lakini ndivyo hivyo alikufa na majibu yote hayo ingawa kifo chake kilizua utata mwingi na sintofahamu, huku wakiwepo watu ambao kamwe usingewaambia Ballali amekufa wakakusikia na kukuamini.

Ni mwaka huu mwandishi wa gazeti la mwananchi Meena ndie alietutegulia kitendawili cha wapi alipozikiwa Ballali,pale alipoibuka na story hiyo ya Ballali kwa kututajia mahala alipozikwa ,akituambia kwamba mtanzania mwenzetu huyo Ballali alizikwa nchini Marekani katika eneo maarufu la makaburi nchini humo linaofahamika kama “Gate of Heaven”mwandishi huyo ama kwa kutumwa ama kujituma alienda mbali zaidi kwa kutuonesha mpaka picha za kaburi la Ballali na makaburi mengine,japo alichofeli ni kushindwa kutuwekea walau picha moja ya mwili wa Ballali ukiwa kwenye jeneza.

Kutoka EPA sasa tuna TEGETA ESCROW, yaani msitu mpya, lakini nyani wakiwa walewale,nikiwa kama mtanzania ninaeguswa na kuumizwa na athari za ufisadi na rushwa za aina yeyote kama wizi wa Richmond, EPA, ESCROW, RADA. Ninaliona zengwe lilioko mbele yetu kama taifa, hapa tutarajie kudanganywa sana, tutarajie kuhamishiwa ajenda na mwisho tutarajie propaganda nyingi kutoka serikalini kuliko ukweli. Lakini naomba nimalizie kwa kuwauliza wahusika wakuu na wahusika wadogo wa sakata la wizi wa fedha za umma kwenye account ya ESCROW na serikali kwa ujumla. Kwamba safari hii je, wezi wa pesa zetu watapelekwa mahakamani? Ama wataumwa gafla na kukimbilia kutibiwa ughaibuni kama alivyofanya Balali? Je, watuhumiwa wakijifisha ama kufishwa watazikwa safari hii nyumbani Tanzania ili nami nipande treni kutoka kwetu Kigoma walau niwahi matanga? Ama ni kama kawaida watazikiwa ughaibuni (Marekani)mnijibu kiungwana tafadhari, watazikwa Bongo ama kwenye makaburi ya Gate of Heaven kama Ballali?

Martin Kadinda 'Kama Wameachana Basi Wamechokana Wenyewe Mimi Sio Chanzo cha Kuachana Kwao'

Posted: 20 Nov 2014 08:01 AM PST

'Oyooooooo...naona now tunaanza kupangiana maisha aiseee... This is my personal page i post about myself and kazi zangu za ushonaji na ubunifu.... Ukiona post about @diamondplatnumz @wemasepetu @officiallulumichael @petitman_wakuache or any other person.. Its because those are my people niko nao mara nyingi ila sio lazima to post anything about them.... So if i post am having sex... Am naked.. Am eating or anything its my page.... GET That.... back to BMW and mahusiano ya hao watu wawili sihusiki na sina taarifa about kuachana kwao... Na kama wameachana watakuwa wamechokana wenyewe.... Mimi niwe chanzo cha kuachana kwao kwakuwa nilikuwa kuwadi wa kuwakutanisha?? Kawa walivyotongozana ndo watakavyoachana.... Tatizo lenu mmekariri maisha na akili za matope kulainika kila mkimwagiwa maji..... Ukijiona ni bingwa wa matusi fungua page yako tukana...... Nasemajeeeeeeee #NdoIshakuwa na mkae mkijua FARASI UMPANDAE AKUTISHI KWA MBIO ZAKE........' Kadinda

Unaweza Kuudownload Wimbo Mpya wa Diamond Uliotoka Leo Hapa

Posted: 20 Nov 2014 05:31 AM PST

Diamond Ametoa Wimbo Mpya Siku ya leo Unaitwa Ntampata Wapi , Kama Unataka Kudownload basi Hapa ndio Mahala Pake..

Maruhani Yamsumbua Penny, Apiga Makelele Barabarani Ovyo

Posted: 20 Nov 2014 05:31 AM PST

Prizenta wa Kituo cha Radio E-FM cha jijini Dar, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ anadaiwa kukumbwa na mauzauza yaliyodaiwa ni mapepo na kujikuta akipiga makelele barabarani.

Habari kutoka kwa shuhuda wetu zilidai kwamba, ishu hiyo ilijiri maeneo ya Makongo jijini Dar es Salaam, juzikati wakati staa huyo akielekea msibani ambapo rafiki yake kipenzi aitwaye Skitter alifariki dunia.

Chanzo hicho kilidai kwamba Penny alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kawaida, alipofika maeneo hayo aliegesha gari pembeni na kuanza kupiga kelele akilia kwa uchungu hivyo kuwaacha watu waliomshuhudia wakiwa midomo wazi wakitaka kujua kilichompata mtangazaji huyo. Mpashaji wetu huyo alizidi kueleza kwamba baada ya kama  dakika kumi, Penny aliondoa gari na kuendelea na safari.

Paparazi wetu aliponyetishiwa ishu hiyo alimtafuta Penny na kumuuliza kuhusu tukio hilo ambapo alisema alikuwa akienda kwenye msiba wa rafiki yake, alipokaribia kufika alipata uchungu ndiyo akatokewa na hali hiyo.

Angalio Video ya Wimbo Mpya wa Diamond-Ntampata Wapi

Posted: 20 Nov 2014 05:23 AM PST

Alhamisi ya Nov 20 Diamond Platnumz  ameibariki siku hii kwa kuachia video na audio ya wimbo wake mpya unaoitwa Nitampata wapi,kwenye radio station,tv na kwenye mitandao.
Video hii ambayo kwa mara ya kwanza ilianza kuonyeshwa Nov 19 kupitia kituo cha MTV BASE,kama hukufanikiwa kuiona unaweza kuiona kwa kubonyeza play hapo chini.

Sina Mahusiano na Sitti Mtemvu- Lundenga

Posted: 19 Nov 2014 09:57 PM PST

Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ni waandaaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na aliyekuwa mshindi wa kwanza wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu.

Lundenga amefunguka hayo leo alipokuwa akichata Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa sita mchana mpka saa nane mchana.
Mbali na mahusiano Watu wengi walitaka kujua ni sifa zipi zilizompelekea mrembo Sitti Mtevu kutwaa taji hilo kama si upendeleo kutoka katika kamati na crew inayohusika kuandaa mashindano hayo kwani watu wengi wamekuwa wakisema kuwa mrembo huyo alikuwa hastahili kushinda taji hilo ukilinganisha na warembo wengine ambao walikuwa wakichuana nae,kufuatia hali Ludenga ikabidi aweke wazi sifa tano amabzo zinamfanya mtu kushinda taji la Miss Tanzania kuwa ni lazima awe na sura nzuri, umbo zuri, mvuto, haiba, ufahamu wa kutosha wa mambo mbali mbali.

SITI HANA SIFA YA KUWA MISS TEMEKE
Kutokana na maamuzi ambayo Sitti Mtevu aliamua kujivua taji la Miss Tanzania 2014 hivyo mrembo huyo amejifutia sifa zake zote alizopata katika kusaka taji la Miss Tanzania hivyo si Miss Chang'ombe wala si Miss Temeke tena.
Hashim Lundenga amesema kuwa kitendo cha Sitti kujivua taji hivyo automaticaly amevua mataji yake yote aliyopata katika ngazi ya wilaya mkoa na hata Taifa kama ambavyo ilivyotangazwa.
"Hashim Lundenga: Automatimacally anakuwa amejivua na mataji mengine pia...."
Kufuatia sakata la Mrembo Sitti Mtevu kudanganya UMMA juu ya umri wake na kumgharimu kulivua taji hilo la Miss Tanzania 2014.Ludenga amesema kuwa hali ya udanganyifu wa umri wa warembo hao huwa ni suala la kawaida na lipo kila mwaka ila kwa kuwa huwa wako makini ndiyo maana wangundua hivyo haoni sababu ya yeye na kampuni yake kuwajibika kisa Sitti Mtevu alidanganya umri.
"Hashim Lundenga: sio sahihi, tupo makini na ndio maana tumegundua, fahamu ya kwamba kila mwaka washiriki wengi tu hutudanganya kuhusu umri wao na ndio maana tupo makini...... tuwajibike kwa kosa gani?????"

NIPO TAYARI KUKABIDHI KIJITI KWA MWINGINE
Kufuatia kuzuka kwa kashfa mbalimbali zinazohushisha mashindano ya Miss Tanzania na waandaaji wake mashabiki wa Eatv walitaka kujua kama Mkurugenzi huyo wa Lino Agency Hashim Lundenga yupo tayari kuachia nafasi hiyo ili watu wengine waweze kuendeleza pale wao walipohishia lakini Ludenga aliweka wazi kuwa yeye kama Mkurugenzi yupo tayari kuchagua mtu mwingine ili asimamie nafasi yake lakini si kuwaachia watu wengine kuendesha shindano hilo.
"Hashim Lundenga :Lino International Agency ni Kampuni ya mtu binafsi na inayo Directors wake, hivyo tunaweza kuteua Mkurugenzi mwingine wa kufanya kazi hiyo........"

MISS TANZANIA HAIWEZI KUFUTWA
Kutokana na baadhi ya watu kutooana umuhimu wa uwepo wa mashindano ya Miss Tanzania na kuyahusisha na kumomonyoka kwa maadili hususani kwa warembo wa Tanzania watu wamependekeza mashindano hayo yafutwe kwani yamekuwa hayana tija na hayana haki kwani kumekuwa na upendeleo na udanganyifu na vitendo vya rushwa ambavyo hupelekea wasichana wengi kuvunja utu wao kwa sababu ya kutaka kushinda au kufikia hatua fulani katika mashindano hayo.
"Hashim Lundenga:Sitty bado ni msichana mrembo na ataendelea kuwa mrembo....haya mashindano hayawezi kufutwa kwa sababu wananchi wanaelewa faida zake, wewe usiyejua faida zake, baki hivyo hivyo..."

MISS TANZANIA HAKUNA FAIDA YOYOTE
Hashim Lundenga ameweka wazi kuwa katika mashindano hayo hakuna faida yoyote anayopata zaidi ya yeye mwenyewe kufahamika na kutembea nchi nyingi duniani,watu walitaka kujua kwanini miaka yoye amekuwa aking'ang'ana yeye tu katika kuandaa na kusimamia mashindano hayo na je anafanya kwa masilahi ya nani na hayo ndiyo yalikuwa majibu ya Lundenga
"Hashim Lundenga hakuna faida yeyote, zaidi ya kufahamika, kutembea nchi nyingi duniani, n.k."

KASHFA YA NGONO KWANGU FITINA TU
Hashim Lundenga amekana leo wakati akichat Live na mashabiki wa ukurawa wa EATV kuwa hana kashfa ya kuomba ngono au kuwa lazimisha warembo hao kutoka na yeye kingono ili waweze kushinda au kushiriki mashindano hayo,Ludenga anasema hizo ni fitina tu za watu fulani wenye lengo la kumchafua na kuchafua mashindano hayo.
"Hashim Lundenga hakuna kashfa kama hiyo..........hiyo ni fitna.............."
Lakini pia Lundenga aliwaambia watanzania kuwa kutokana na Sitti kujivua taji na kumpa nafasi mshindi wa pili kuchukua taji hilo hivyo wasitegemee tena sherehe za kumkabidhi taji hilo Miss Tanzania namba mbili kwani shehere watafanya wazazi wake pamoja na wakala wake wa mkoa alipotokea
"Hashim Lundenga hakuna sherehe yeyote, sherehe huandaliwa na wazazi wake na wakala wake wa mkoa alipotokea"
Hashim Lundenga alimaliza kwa kusema kuwa tunaoomba radhi sana kwa wale wote ambao hatukuweza kujibu maswali yenu yote kutoka na ufinyu wa muda.

Kaka Yangu Anataka Kumuoa Mchumba Wangu, Ameamua Kwelikweli

Posted: 19 Nov 2014 09:35 PM PST

Ndugu zangu kuna mchumba wangu mpaka sasa tuna mahusiano yenye umri wa miezi 5. 

Kaka yangu wa damu amekomaa kumchukua na kibaya jana kaniwahi kwenda kumtolea mahari(kiukweli kimapato ameniacha gepu sana), ndugu wa binti wamempokea tena vizuri. 

Nikimuuliza mchumba wangu kuna nini tena? Anadai naye hailewi kinachoendelea na ananishauri niwaishe mahari ndani mwezi huu.

Nikimuliza unamtaka nani ? Anadai amechanganyikiwa katika hili swala ila anadai kuwa bado ananipenda.

Ndugu zangu nifanyeje katika hili?

Zitto na Kafulila Walibezwa na Kudhallilishwa je Waliowadhalilisha leo Wanajisikiaje?

Posted: 19 Nov 2014 09:30 PM PST

Kiukweli nilisikitika sana pindi nilipoangalia bunge na kumsikia AG akimdhalilisha Kafulila kwa kumuita tumbili ulikuwa ni ubaguzi wa hali ya juu mwafrika kumuita mwafrika mwenzake tumbili tunayaona ulaya tu tena kwenye mchezo wa kandanda.AG huyu hakuishia hapo akamtisha na kukiondoa kichwa chake.Siku zikifuata tukamsikia katibu mkuu mwenye jeuri ambaye kafukuzisha mawaziri wengi kazi sababu ya upigaji wake akaibuka na kuwabeza Zitto na Kafulila kuwaita wala rushwa na kukazia hawa ni tumbili na wana makaratasi ya kufungia maandazi wanajidaia kinga ya bunge watoke nje kama ni wanaume kweli niwaoneshe na kutoa vitisho vingi na kujinasibu yeye ni msafi.Sasa wazee ripoti ipo mezani tunasubiri tuone usafi wenu sasa bwana katibu na AG

Navio Awakubali Wakali Bongo Flava Tanzania..Ataja Msanii Anaye Taka Kufanya Nae Wimbo

Posted: 19 Nov 2014 09:49 PM PST

Rapa mkali kabisa kutoka Uganda, Navio ambaye kwa sasa yupo hapa nchini Tanzania kwa shughuli za kimuziki, amewataja wasanii Shaa, Diamond, Joh Makini, Izzo Business, Vanessa Mdee na AY kama wasanii kutoka hapa Bongo ambao anawakubali zaidi.

Navio ameiambia eNewz kuwa, kazi za wasanii hawa pamoja na moyo wao katika kazi ni kati ya vitu vinavyomfanya kuwaelewa zaidi pamoja na kufurahia kazi zao.
Rapa huyo pia ameweka wazi uwezekano wa kufanya kolabo na wasanii kutoka hapa Tanzania, akiwa tayari katika maongezi ya awali na msanii Izzo Business.

CUF Kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Posted: 19 Nov 2014 09:22 PM PST

Chama cha Wananchi CUF kimesema kitasusia uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwaka huu kama serikali (TAMISEMI) haitabadilisha kanuni za uchaguzi huo ambazo anadai kuwa zina lengo la kuvikandamiza vyama vya upinzani.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CUF Tanzania bara Magdalena Sakaya amesema serikali ya Tanzania imekurupuka kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu kwani haikuwa na mpango kamili kuendesha uchaguzi huo.
Sakaya amesema viongozi wa serikali wamekuwa wakitoa taarifa zinazokinzana juu ya uchaguzi huo kati ya Rais na Waziri Mkuu, ambapo Rais alisema katika kikao cha mashauriano ya vyama vya siasa kilichoandaliwa na TCD kuwa uchaguzi huo ungefanyika mwezi Februari mwakani na Waziri Mkuu kutangaza kuwa uchaguzi huo utafanyika
Desemba 14.
Kwa upande wa kiongozi wa CHADEMA bwana Fulgency Mapunda ambaye ni Afisa uhamasishaji Chadema amewataka viongozi wa halimashaurui zote kuacha kuwakandamiza wagombea wa upinzani kwa mashinikizo ya viongozi wa kisiasa.
Naye Diwani wa Kigogo kupitia CCM Richard Chegula amewataka viongozi wa upinzani wkuacha lawama kabla ya uchaguzi kwani waamuzi ni wapiga kura wenyewe.
Kwa upande wa Tamisemi kupitia Mkurugenzi wake wa serikali za mitaa bwana Calist Luanda amefafanua juu ya swala zima la uchaguzi huo, na kusema kuwa tuhuma zinazotolewa siyo za kweli

Halima Kimwana Akana Kuhusika na Uhusiano wa Diamond na Zari

Posted: 19 Nov 2014 09:19 PM PST

Mdada wa mjini ambaye ni dada wa hiyari wa msanii, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Halima Kimwana amedai kuwa hahusiki na uhusiano unaoendelea kati ya kaka yake huyo na mrembo kutoka Uganda, Zari.

Akizungumza na waandishi wetu, Halima alisema kuwa hawezi kuzungumzia suala lolote la Diamond na uhusiano wake na Zari kwa kuwa hahusiki na jambo lolote kati yao.

“Jamani mimi sifahamu chochote na siwezi kuzungumzia kwa kuwa sijui na sihusiki,” alisema Halima anayedaiwa kumuunganishia Diamond kwa mademu kibao japo tuhuma hizo anazipinga.

Wema Sepetu Aanika Kisa cha Kumwaga Diamond Platnumz

Posted: 19 Nov 2014 09:14 PM PST

Na Musa Mateja
MISS Tanzania 2006/07 ambaye ni staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’, amevunja ukimya kwa kuamua kuanika kisa cha yeye kummwaga aliyekuwa mwandani wake, nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Akizungumza na Amani katika mahojiano maalum jijini Dar, juzikati, Wema alianza kwa kufunguka kwamba, kuna watu wamekuwa wakizungumzia ishu ya yeye kumtema Diamond huku kisa wakiwa hawakijui na wengine wamehamishia sababu kwa nyota wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’, jambo ambalo si kweli.

Wema alimwaga ‘ubuyu’ kwamba, yeye ameamua kumpa likizo ndefu Diamond ili kila mmoja aweze kufanya mambo yake ya maana kwa uhuru mkubwa hasa baada ya jamaa huyo kunukuliwa na magazeti pendwa akisema hana mpango wa kuoa jambo ambalo lilimkatisha tamaa na kumwacha njia panda.

SAFARI YAKE CHINA NAYO TATIZO
Kuhusu suala la kusema amempa likizo ndefu ili kila mtu afanye mambo yake,
Wema alirejea safari yake ya China hivi karibuni ambapo Diamond hakutaka asafiri ila akalazimisha. Hapo aliona anatakiwa kuwa huru zaidi.

MWISHO WA LIKIZO
Wema alipotakiwa kutaja mwisho wa likizo hiyo endapo ni ya siku 28  kama ilivyo
kwa sheria ya kazi ya Tanzania, aligoma kusema chochote huku akisisitiza amempa likizo Diamond.

AMZUNGUMZIA ZARI
Staa huyo asiyekaukiwa na matukio, alikwenda mbele zaidi kwa kumzungumzia Zari ambapo alisema kuna wanaodai mwanamuziki huyo tajiri yuko kimapenzi na Diamond, lakini yeye haoni ukweli wowote kwani anajua wawili hao wana ‘projekti’ ambayo ni mawazo ya muda mrefu.

BOFYA HAPA KUMSIKIA WEMA
“Kwanza naomba watu wajue kuwa, projekti ya Diamond na Zari ninaijua na bahati nzuri Zari ni shoga‘ngu tangu kitambo hivyo yote yanayofanyika mimi nayatambua hatua kwa hatua pamoja na kwamba sijaongea na Diamond siku nyingi,” alisema Wema.

DIAMOND AULIZWA KAMA ANAITAMBUA LIKIZO NDEFU
Baada ya mazungumzo na Wema, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond kwa lengo la kutaka kumfahamisha kama anafahamu kwamba amepewa likizo ndefu.
“Dah! Nashindwa niseme nini hapo! Lakini ujue maisha kila mfa maji siku zote haishi kutapatapa, kiukweli mimi hapo naona Wema anatoa majibu ya kisiasa tu.

“Nashindwa kujibu kila linalosemwa na watu ila kuna kipindi mtu hutakiwi kujibu kila kitu. Kuna mambo mengine yanatakiwa uyaache yapite tu.
“Mimi nimeachwa na Wema, Zari ni rafiki yangu tu, acheni projekti iendelee,” alisema Diamond huku akichekacheka kwa ishara ya furaha akijiandaa kuachia ngoma kali mpya iitwayo ‘Nitampata Wapi’ leo.

KWENYE WHATSAPP
Wakati Diamond akisema hayo, baadaye kwenye maelezo yake mafupi (profile) ya WhatsApp aliweka picha ya Zari huku akiambatanisha na maneno yaliyosomeka:
“Unapokosa usisikitike, Mwenyezi Mungu kakuandalia kizuri zaidi.”

Wema na Diamond wamekuwa na kasumba ya kuachana na kurudiana hivyo kuna kila dalili wawili hao wakarudiana tena.

It’s All Love: Wema Sepetu na Penny Wafanya Shopping Pamoja

Posted: 19 Nov 2014 08:05 PM PST

Walikuwa marafiki wa damu, wakaja kuwa maadui.. na sasa ni marafiki tena. Baada ya kupatanishwa kwenye sherehe ya kuzaliwa ya Junaithar siku kadhaa zilizopita, Wema Sepetu na Penny Mungilwa wameendelea kuuimarisha zaidi urafiki wao.

Penny ameshare picha kwenye Instagram akiwa pamoja na Miss Tanzania huyo wa zamani ambayo Wema pia ameirepost kwenye akaunti yake. Hiyo ni picha ya kwanza ya warembo hao wakiwa pamoja kuwahi kuweka kwenye akaunti zao katika kipindi kirefu.

Wakiongea kwa pamoja na Bongo5 leo wakifanya shopping ya nguo, warembo hao wamedai kuwa wana mipango ya kufanya filamu pamoja na wanatarajia kuingia kambini mwakani.

Picha hiyo imepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wao wanaopenda kuwaona wakiwa pamoja.

Udaku Specially

unread,
Nov 21, 2014, 4:34:34 PM11/21/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Penny Ataja Mahari Yake Kwa Mtu Atakae Taka Kumuoa

Posted: 20 Nov 2014 09:42 PM PST

Jina la Penny limo katika orodha ya mastaa waliowahi kuwa na uhusiano na msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’. Jina lake kamili ni Penniel Mwingilwa. Huyu ni Mtangazaji wa Radio Efm ya jijini Dar.


Wiki hii yuko hapa kujibu maswali ambayo waandishi wetu Imelda Mtema na Hamida Hassan walimuweka mtu kati.Ijumaa: Mambo Penny, naona sasa hivi una gari nyingine, ile Toyota Brevis ambayo mpenzi wako wa zamani Diamond alikununulia iko wapi?

Penny: (Kicheko)...kwa kweli namshukuru kwa kuninunulia ile gari ila sasa hivi siko nayo, nimeamua kubadilisha, si unajua mtu lazima uende na wakati?
Ijumaa: Mara ya mwisho kupanda daladala ilikuwa lini?

Penny: Nakumbuka ilikuwa mwaka 2008. Nilipoanza tu kazi ya utangazaji, nilipopanda daladala watu walikuwa wananishangaa sana nikaona hiyo siyo poa, nikawa napanda teksi.

Ijumaa: Ulikuwa na Diamond mkaachana, hebu tuambie kwenye maisha yako ungependa umpate mwanaume wa aina gani?Penny: Kwanza awe mchamungu, pili anithamini lakini pia awe mtu muelewa. Yaani ajue ni wakati gani wa kufanya maamuzi sahihi na awe tayari kunisikiliza.

Ijumaa: Nini ambacho kinakukwaza sana na hukipendi kabisa?
Penny: Ni watu kuniongelea tena kwa mambo ambayo hawayajui kuhusu mimi. Nakerwa sana na wanaofanya hivyo.Ijumaa: Ukiwa katika ‘stress’ au mtu kakukwza na kukukosesha amani, kipi ambacho huwa unakifanya kurudisha amani yako?

Penny: Nikiwa katika hali hiyo breki ya kwanza ni kanisani. Pale kwenye Kanisa la St. Joseph pembeni kuna kakanisa kadogo.Kwa hiyo nakwenda pale, nasoma Biblia na kusali kwa muda wa saa sita hivi kisha nikiondoka hapo nakuwa sawa.

Ijumaa: Muda wa kuolewa ukifika na mwanaume akaja kwenu na ukatakiwa utamke mwenyewe mahari yako, ungetaka mahari ya shilingi ngapi?Penny: Sina makuu, nitamtaka mwanaume huyo ampe baba yangu juzuu na msahafu halafu mama yangu apewe Biblia. Kama kutakuwa na pesa kidogo tutaipeleka kwa watoto yatima.

Ijumaa: Mastaa wengi wa kike wanadaiwa kutojua kupika, wewe hili likoje kwako?
Penny: Kitu ambacho nitamshukuru mama yangu siku zote ni kunifundisha kupika. Najua kupika vitu vingi sana tena vinakuwa vitamu mno, kasoro ugali ndiyo unanishinda ila najitahidi kujifunza.

Ijumaa: Umeanza kujitegemea ukiwa na umri mdogo, vipi unajilindaje na vishawishi vya wanaume?
Penny: Wakati naanza kupanga tulikaa kama familia, tukajadili ikaonekana naweza kukaa peke yangu japo bado nipo chini ya wazazi wangu. Kuhusu vishawishi havinisumbui kwani najitambua.

Ijumaa: Kilichowasukuma mkaamua kupatana na Wema Sepetu ni kipi?
Penny: Sisi ni watu wazima, tuliona haileti picha nzuri kuwa maadui. Sasa hivi tuko na amani na hatutaruhusu watu watugombanishe tena.

Ijumaa: Ni kwa nini unapenda kuvaa nguo fupi?
Penny: Vimini siwezi kuacha ndugu yangu kwa sababu nina mguu mzuri wa kuvaa hivyo, au wewe unanionaje?

GPL

Baada ya Shy-Rose Bhanji Kudaiwa Kumpiga Mbunge Mwenzake, Hiki Kimesemwa ungeni

Posted: 20 Nov 2014 09:40 PM PST

Kumekuwa na taarifa kuhusu kuwepo migogoro mbalimbali inayohusisha Wabunge wawakilishi wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki ambapo Mbunge Shy-Rose Bhanji amehusishwa sana kwenye vichwa vya habari.
Kwenye kikao cha Bunge November 20 2014 Dodoma Hatibu ambae ni mbunge wa Zanzibar aliuliza 
 “… Sisi wabunge wa bunge hili ndiyo wapiga kura wa kuwachagua wawakilishi wetu wa kutuwakilisha katika bunge la Afrika Mashariki, kumekuwa na taarifa za kulipaka Taifa hili matope kulitia aibu kutokana na  baadhi ya wawakilishi wetu, Wabunge wetu wa Afrika Mashariki kutokana na matendo wanayoyafanya kule..”

“…Ni lini hasa kinachoendelea pale na hatua gani zilizochukuliwa kuhusu ukosefu wa nidhamu uliojitokeza kwa mbunge Shyrose Banji wazi wazi na bili hali hakuna taarifa yoyote, Mheshimiwa Naibu Spika naomba mwongozo wako…”– Hatibu.

Baada ya swali waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akawasha kipaza sauti na kutoa haya majibu “…Naomba nitoe taarifa kwamba kinachotokea katika Bunge la Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa  spika mwenyewe, hilo ndiyo chanzo cha matatizo mengi, kwa hiyo  wabunge  wa Bunge la  Afrika Mashariki wamegawika kataka makundi mawili, kuna kundi linalotaka Spika lazma aondolewe, na wengine wanadai wanamtetea abaki…”

Sasa katika kundi ambalo wanataka  abaki imeonekana Tanzania ndio kikwazo, kwa sababu ili upate uamuzi ndani la Bunge la Afrika Mashariki  katika suala lolote lazima upate akidi inayotosheleza kutoka  kila nchi, sasa wabunge wa Tanzania ambao mwanzoni waliunga mkono hoja ya kumuondoa yule Spika wamefuta hilo na wamekubaliana aendelee kwa hiyo imeleta chuku kiasi Fulani…“– Sitta.

 “…Katika tukio ambalo limetokea juzi na nasema hivi kwa sababu  Naibu Waziri wangu yuko kule kwa hiyo ni jambo halisi, kilichotokea sio kama kinavyoelezwa Mheshimiwa Shyrose Banji ambaye anahesabika ni mfuasi mkubwa wa Yule Spika kiasi kwamba wenzie wanamuona kama kibaraka vile, alikuwa anapita katikati ya Wabunge wengine kuwahi usafiri kwa bahati mbaya akamgonga Mheshimiwa Ndelakindo Kessy, Mheshimiwa Ndelakindo akahamaki na kwa kusaidiwa na  baadhi ya Wabunge  wengine wa Uganda akaenda kituo cha Polisi kutoa taarifa kwa madai kwamba amefanyiwa makosa ya jinai wanaita ‘assaults’…“– Sitta.

Wazazi wa Miss Tanzania Mpya Wacharuka..Wahoji Zawadi za Mtoto wao Zipo Wapi

Posted: 20 Nov 2014 09:27 PM PST

 Wazazi wa Miss Tanzania mpya, Lilian Kamazima wameitaka Kamati ya Miss Tanzania  iwape maelezo ya uhakika kuhusu zawadi na taji la binti yao kwa kuwa hadi sasa wako njiapanda.

Kauli hiyo ya  Eva na Deus Kamazima imekuja siku chache baada ya mrembo huyo kuwasili jijini Arusha akitokea Dar es Salaam.

Wakizungumza nyumbani kwao, Majengo Juu jijini Arusha jana, wazazi hao walionyeshwa kushangazwa na hatua ya kumpokea binti yao akiwa hana taji, pamoja na fedha ambazo alistahili kupatiwa kama mshindi.

Walisema kuwa walimpokea binti yao kama ‘yatima’, hata tiketi ya ndege alilazimika kulipiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwandago Investment Ltd, aliyemuibua katika ngazi ya Kanda ya Kaskazini.

“Tunaiomba Kamati ya Miss Tanzania itupe maelezo ya kina kuhusu zawadi, taji pamoja na vitu vingine kwa kuwa tumempokea binti yetu kama bila zawadi wala taji,” walieleza wazazi hao kwa nyakati tofauti.

Awali, mrembo huyo alisema kuwa pamoja na kwamba bado hajakabidhiwa taji wala zawadi yoyote na Kamati ya Miss Tanzania, lakini kitendo cha kupewa kiti hicho ameridhika.

“Sijapewa taji wala zawadi , lakini kitendo cha kupewa kiti cha umalkia nimeridhika,” alisema  Lilian.

Mkurugenzi wa  Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga alipoulizwa kuhusu madai hayo alisema kuwa ni kweli bado hawajamkabidhi fedha na zawadi  kwa kuwa kuna taratibu za kiofisi bado zinafanyika.

“Ni kweli, tulimwambia atuachie akaunti yake kwa kuwa kuna taratibu zinafanyika, tutamwekea pesa na kuhusu zawadi huyo alirithi taji, hakuwa mshindi wa kwanza, lazima mwelewe,” alisema Lundega.

Udaku Specially

unread,
Nov 22, 2014, 4:39:53 PM11/22/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Ukweli Kuhusu Safari ya Jaji Mkuu Washington DC, Maafisa Wake na Francis Nyalali

Posted: 22 Nov 2014 03:14 AM PST

Tumefanya uchunguzi hapa DSM na huko Washington DC kufuatilia hicho kinachoitwa semina ya majaji
iliyofanyika USA ambayo ilijaza na maafisa wakuu wa mahakama. uchunguzi wetu ulianzia ubalozi wa marekani 
hapa dsm eneo la Drive inn kupata ukweli juu ya semina ya majaji hao lakini ktk kitengo chao cha habari kwa
Bw. MOORE akatuambia hakuna kitu kama hicho kuhusu mualiko wowote unaousiana na semina ya majaji au wanasheria uliopita ubalozi huo.

Tukatoka hapo tukawasiliana na ubalozi wa Tanzania uliopo washington DC kupata maelezo yeyote kuhusiana na semina yeyote ya majaji inayoendelea huko ofisa wa ubalozi alisita kwanza lakini baadaye walituambia kuwa hawawezi kushea information kama hizo na sisi kwahiyo tuwasiliane na wausika. Tukaenda kwenye website ya mahakama kuu ya marekani kuona kama kuna tangazo lolote kuhusu semina hakuna kitu kama hicho tumekuta matukio mengine lakini hakuna issue ya semina. Tumewasiliana na wahusika akiwemo jaji mmojawapo kwy ule msafara simu zao zinaita hazipokelewi.

Conclusion yetu

Kulingana na uchunguzi wetu tumeitimisha kuwa jaji mkuu pamoja na maofisa wa mahakama walikwenda Washington DC kwa ajili ya kitu kimoja tu nacho ni kujadili suala zima la issue ya acount ya Escrow na mpaka hivi sasa hakuna ushahidi wowote kuhusiana na uwepo wa semina unless watoe picha zinazoonesha semina hiyo ambayo wahusika walidai walikwenda kuhudhuria na siyo kuonana na JK.

Swali kubwa ambalo inabidi watanzania tujiulize hivi ni kweli mahakama zetu ni huru ?? kwa mujibu wa uchunguzi wetu ni kuna muingiliano wa hali ya juu kati ya mahakama na executive kwa maana ya ikulu. Tunajiuliza kama jaji
mkuu na maofisa wa ngazi ya juu wa mahakama wanaweza kufunga safari kwenda kuonana na Rais kwa ajili kujaribu kupotosha nchi na kulinda mafisadi. Je Rais anapokuwa nyumbani ni mara ngapi jaji mkuu na maofisa wake wanakwenda ikulu kujadili na mkuu wa nchi kuhusu mienendo ya kesi mbali mbali na maswala ya ushahidi?? 

Hii inatupelekea kuamini kabisa maneno aliyoongea aliyekuwa jaji mkuu wa Tanzania Francis Nyalali kuwa mahakama za Tanzania si huru na zitakuwa huru tu endapo ikulu itakapoacha kuitisha na kuyajadili mafaili ya watuhumiwa ikulu.

Kitendo cha ofisa wa ngazi ya juu wa ikulu Bw.Ombeni Sefue cha kutoa tamko la kutojadiliwa issue ya ESCROW bungeni na kujigeuza messenger wa mahakama na kulitishia bunge kuwa linaingilia amri ya mahakama ni kosa la wazi na linathibitisha jinsi ikulu inapoingilia wazi uhuru siyo wa bunge bali na mahakama zetu.

By  Politiki/Jamii Forums

Jokate: Mimi Sio Malaya Jamani

Posted: 22 Nov 2014 12:20 AM PST

MWANAMITINDO na mtangazaji kiwango Bongo, Jokate Mwegelo amefunguka kuwa sababu kubwa inayomfanya awe karibu zaidi na wanaume ni marafiki zake wa kike kuwa nje ya nchi .

Akizungumza na mwanahabari wetu, Jokate alisema amekuwa akipata malalamiko kutoka kwa watu wengi kuwa kampani yake kubwa ni wanaume hadi wengine kumuona ni malaya wakati si kweli .

“Watu wengi wanasema mimi malaya kwa sababu ya ukaribu wangu na wanaume lakini ukweli ni kwamba kampani yangu ya kike kubwa ipo nje ya nchi , sina jinsi, ” alisema Jokate.

Mwenzangu Embu Angalia Hii Kitu Jinsi Wenye Nchi Wanavyogawana Mabilioni ya Fedha Huku Hospitalini Hakuna Dawa

Posted: 22 Nov 2014 12:18 AM PST


Picha Hapo Juu ikionyesha Mgawanyo wa Fedha.....

Mwee....Hapana sio kila siku ni jumapili .siku nyingine ni ijumaa wakishindwa tutaingia mtaani kudai haki zetu .pamoja na ukawa tunaweza sio kitu ,ushenzi kama huu unatakiwa ukomeshwe ili tufike tnako taka kwenda watu wachache wanagawana hela ya kusambaza madawa nchi nzima huu ni uonevu wa wanyoge hatukubali..

Hili Sakata la ESKROW ni matata matupu.
1. Ziara ya Jaji Mkuu kwenda kumtembelea Mh. Rais (nini ulikuwa mjadala)?
2. Maamuzi ya kusema Sakata hili lisijadiliwe Bungeni liko Mahakamani... Je linatokana na Ziara?
3. Waziri Mkuu kutaka Busara itumike. Ipi? labda angetoa ufafanuzi...
4. Wabunge kutoridhishwa na mwenendo wa Sakata na na namna Serikali inavyotaka kulifunika funika.
Spika uamuzi wako utaliokoa Taifa au kulididimiza. Ni wazi kabisa ukumbuke hapo ulipo utakachokifanya kitadhihirisha umoja wa uovu au weledi wako kupingana na maovu..

Hatimaye Diamond Aongelea Kuhusu Kuachana na Wema na Mahusiano yake na Zari Boss Lady

Posted: 21 Nov 2014 11:57 PM PST

Jana Nov 21, Diamond amesikika kwenye show ya XXL ambapo amezungumzia mambo mengi, baadhi ya yale aliyoyazungumzia ni pamoja na story zilizoenea mitandaoni kwamba mahusiano ya msanii huyo na Wema yameisha pamoja na story ambayo imetokana na kuenea kwa picha mitandaoni za msanii huyo na Zari the Boss Lady kutoka Uganda.
Hii ni sehemu ya mahojiano aliyofanya Diamond kwenye XXL:

Adam Mchomvu :”…Nataka kujua ile vibe ya Fiesta that day, story zilikuja ooh Diamond kazomewa.. kazomewa kazomewa..na vitu kama vile, sijapata chance ya kukusikia wewe una kipi cha kuzungumzia kuhusiana na that situation..?“

Diamond :- “… Siku zile kwangu ilikuwa kama mchezo, unajua muziki ushakuwa kama sio fani tena, ushakuwa kama siasa.. So, lazima uichukulie hivyo wewe mwenyewe kama msanii ujue una control vipi kwa sababu sio mara ya kwanza vitu kama hivyo vishatokea Maisha.. Maisha yalitupwa mpaka na mayai viza kabisa.. Ni vitu ambavyo vikitokea naonaga kama ni kawaida…“

B 12  :-“…Kwa hiyo ukweli uko wapi kati yako wewe na Wema Sepetu?...”

Diamond  :- “…Kuna vitu vitu fulani nadhani kuvizungumza sio vizuri… Lakini ikifikia kuvizungumzia vinazungumziwa… Uzuri wa mahusiano yetu ni kwamba kila mtu anafahamu… Haijafikia kuweka wazi ndio maana ninapoulizwa inakuwa ni swali gumu kulijibu.. “

B 12 :- “.. Ni gumu kwa upande wako lakini yeye yuko tayari kuzungumza kwamba it’s over kati yangu mi’ na Diamond…“

Diamond  :- “… Sijui…“

B 12  :- “...Hii ngoma kama umemzungumzia yeye direct hivi… watu wamekuza akili zao zikaenda mbali zaidi kimawazo lakini, kwamba inawezekana ile singo umemwimbia yeye hivi kwamba bado unamzimia japokuwa bado kama kakutosa hivi…“

Diamond  : “.. Waswahili wanasema ‘A’ na ‘B’ yote majibu, halafu ukisikiliza ile nyimbo kama kweli mtu mwenye ufahamu wako, kweli kabisa hauwezi kuwa na maswali mengi …“
Kuhusiana na mahusiano yake na Zari the Boss Lady, Diamond amejibu hivi:

Diamond  :- “.. Zari ni rafiki yangu tu, alipokuja hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake Tanzania na kama mimi ndiyo mwenyeji sikutaka kuleta roho za kibaguzi, unajua hata alipokuja Davido pia ilibidi awe na mimi karibu ili hata kesho na kesho kutwa  mimi nikiwa Nigeria basi Davido anipokee hivyo hivyo…“

Iko hapa full Interview ya Diamond kwenye XXL, unaweza kuisikiliza kwa kubonyeza play.


Mchezaji Adebayor Adai Mamaake ni Mchawi, Amfukuza Nyumbani

Posted: 21 Nov 2014 11:50 PM PST


Mshambuliaji wa kilabu ya Totenham nchini Uingereza Emmanuel Adebayor amekosana na mamaake kwa madai kwamba anatumia uchawi kumharibia kazi yake.

Duru zimearifu kuwa mama huyo tayari ameondoka katika nyumba ya familia huku dadaake Adebayor akiambia radio moja ya mjini Accra kwamba Adebayor ndiye aliyemfukuza.
Lakini mchezaji huyo wa zamani wa kilabu ya Arsenal anadai kwamba mamaake aliondoka mwenyewe na kwamba hawana mawasiliano yoyote kati yao kwa kuwa amekuwa akitumia uchawi kutaka kumuharibia kazi yake.
'' Ninawezaje kuzungumza na mama ambaye yeye na dadaangu wamekuwa wakijaribu kuniroga''aliwauliza maripota.
Mchezo wa Adebayor katika kilabu ya Tottenham umeathirika katika kipindi cha miezi kadhaa iliopita huku Tottenham ikidaiwa kujaribu kumuuza kwa mkopo mchezaji huyo katika dirisha la uhamisho mnamo mwezi January kufuatia kushuka kwa mchezo wake.

Kama Ulipitwa Kuangalia Wema Sepetu 'In My Shoes' Season Two Basi Hii Hapa Nimekuletea

Posted: 21 Nov 2014 11:45 PM PST

Ule msimu wa pili wa Reality show ya Wema Sepetu In my shoes umeishaanza na hii ndio episode ya kwanza iliyo muhusisha Diamond ndani yake…



Video Hii Hapa:

Umeona Video Nzima ya Jinsi Mfanyakazi wa Ndani Anavyomtesa Huyu Mtoto na Kumpa Kipigo

Posted: 21 Nov 2014 11:30 PM PST

Kama kutakuwa na list ya watu wasio kuwa na huruma hata kidogo ama kwa lugha nyingine tunaweza kusema katili basi bila shaka huyu dada wa kazi kwenye top 10 atashika nafasi ya kwanza…
Hii inawahusu sana wakina mama ambao uwaachia watoto wao Dada wa nyumbani (HOUSE GIRL) pengine kutokana na majukumu ya kikazi au inapotokea safari ya ghafla… hii video itakuonesha tukio zima na tabiwa kama hii wapo baadhi ya Madada wanazo ivyo umakini mkubwa unatakiwa.

Hivi Ndivyo Whatsapp Imevunja Ndoa ya Wawili Hawa

Posted: 21 Nov 2014 11:16 PM PST

Wiki chache baada ya WhatsApp kutambulisha mfumo mpya ambapo iwapo unamtumia message mtu inakuonyesha alama ya tick mbili za kijani na pia inaonyesha muda ambao mtu uliyemtumia message hiyo ameisoma, tayari kuna ndoa ambayo imeingia matatizoni kutokana na hilo.
Mwanaume mmoja Saudi Arabia ametoa talaka kwa mkewe kutokana na kitendo cha mwanamke huyo kutokujibu message aliyomtumia WhatsApp.
Mwanaume huyo amesema kitendo kilichomkasirisha zaidi ni pale aliporudi nyumbani na kumkuta mke wake akiwa busy anachat na marafiki zake kupitia mtandao huo wakati message aliyomtumia yeye hakuijibu.

Jamaa huyo ameona kama kitendo hicho ni dharau kubwa na hakuwa tayari kuendelea na ndoa hiyo ambayo imedumu kwa miaka miwili tangu ifungwe.

Maskini Kijana Sande Aliyekuwa na kilo 250, Amefariki Dunia, Mashirika ya ndege Yachangia Kifo Chake

Posted: 21 Nov 2014 11:12 PM PST

Kijana Sande Mrema aliyekuwa na tatizo la kuwa na kilo nyingi zilizokuwa zikifikia 250 na umri wa miaka 25 aliyekuwa eneo la karakana katika moja ya Hoteli alipokuwa akiishi wakati akisubiri kupatikana kwa Ndege amefariki dunia usiku wa saa nne kuamkia leo jijini Dar es salaam.

Sande amefariki dunia wakati bado taratibu za kuona ni namna gani atakavyoweza kupatiwa ndege kwaajili ya kwenda kupatiwa matibabu nchini india zilikuwa zikifanyika miongoni mwa wanandugu.

Sande Mrema alishindwa kusafiri kwenda nchini india katika matibabu yake baada ya kushushwa mara kadhaa kwenye ndege za kimataifa anazotakiwa kusafiria licha ya ndugu zake kulipa Gharama zote za usafiri wake.

R.I.P Sande.

Unapoufurahia Ujuzi wa Mpenzi Wako, Hujiulizi Kautoa Wapi?

Posted: 21 Nov 2014 10:55 PM PST

Kwetu tunaamini mchawi aliyekubuhu, ni yule aliyeuwa watu wengi zaidi. Au hata ukimuona dereva anakimbiza gari barabarani unaamini ana uzoefu wa udereva wa mda mrefu na atakuwa ameshawahi kuendesha magari mbali mbali.
Sasa linapokuja swala la mahusiano, ninaona watu wanalalamika kuhusu ujuzi wa wenzi wao. Ingekuwa mimi, endapo mwenzi wangu angekuwa na kiwango kidogo cha ujuzi kwenye maswala ya chumbani, lingekuwa jambo la furaha na kheri. 
Pale unapotaka mpenzi wako awe na ujuzi wa PhD katika maswala ya chumbani, wewe unataka awe amejifunzia wapi? Kama unataka mjuzi, nenda kachukue Changu doa ambaye anajua michezo yote...
Dada zetu waliofunzwa wakatulia, na kaka zetu au wadogo zetu waliofunzwa wakatulia technically watakuwa na ujuzi mdogo na over the time katika maisha yao ya mahusiano (ndoa) wataweza kujifunza na kuimprove.
Ukimpata yule anayekupeleka puta, inabidi ukae chini na ujiulize atakuwa amewapitia au amepitiwa na wangapi mpaka akapata utaaalam huo?

NB: Sio wote wenye utaalam wa chumbani wanahistoria ndeefu (mbaya) ya kwenye mahusiano...

Kikao Cha Dharula: Kitimoto kwa Wabunge wa CCM Wanaopigia Kelele Escrow

Posted: 21 Nov 2014 10:49 PM PST

Kikao kinaongozwa na Wasira na Lukuvi, 

Wabunge wa ccm wale wanaopiga kelele kuhusu Wizi huu wamewekwa mtu kati,

Kinafanyikia Ikulu ya Dodoma kwa siri kubwa, hata magari yao yote yameigizwa ndani kabisa, kwa hapa nje lipo Gari la Lembeli aina ya Range Rover Namba T382 lililokosa nafasi ndani. kikao hiki kimeitishwa kwa meseji tu hii ni baada ya jioni kutangazwa kuwa kimeahirishwa,

Sababu za usiri huu ni pale tulipowaanika jana katika kikao chao cha shinikizo kwa Werema ajiuzuru, Zigo limemdondokea Godfrey Zambi kuwa ndie aliyevujisha siri ile kwakuwa aligoma kuzima simu na alikuwa akichati fb wakati kikao kikiendelea, hivyo kikao cha sasa hivi katupwanje.

Kikao hiki kwa sasa kimembana Ndugai kwamadai anaihujumu serikali, 

Ndugai amezila kuendelea na Bunge amesema yeye sasa hata ongoza vikao, bora awe pembeni kuepusha msongamano!

Ccm imegawanyika makundi matatu, lile linaloshinikiza waliohusika na wizi huu wote wapigwe chini lakini,ukifuatilia kundi hili linavizia vyeo vya uwazili, na tayari kampenzi za kuwania vyeo hivyo zimeanza. 

Kundi la pili hili ni wanafiki wa kati wasio na msimamo, lenyewe linataka wafukuzwe wachache (maswi,tibaijuka,mhongo na werema) hili linasema linanusuru serikali isianguke.

Kundi la mwisho ni la wezi wenyewe, hili linafanya kila njia ripoti hii isisomwe bungeni, hili linaongozwa na Pinda na Werema.

UPDATES.22/11/2014

Ndege ya serikali ipo hapa Dodoma imekuja alfajiri hii 5-H CCM.. Aina ya folker F28 haijajulikana imemleta au imekuja kumchukua Nani, ila taarifa za awali zinasema Bilali alikuwa aje leo.

Hali ya mambo ni ngumu kama vile nchi ipo vitani...!

Kinana tayari ameletwa na Ndege mida hii,

Mrejesho wa Kikao Cha jana usiku

Imeamriwa popote alipo Spika Makinda aje, Ndugai out hadi sakata lipite, afanye awezavyo Pinda apone,.. Wachangiaji wakali wasipate nafasi iitwe briefing ya wabunge wote watapike nyongo nje ya waandishi ili siku ya mjadala kuwe na hewa safi.Kama ni kuondoka waondoke mawaziri ila sio waziri mkuu.

Inatakiwa njia ya kumuangukia au kumdhibiti Mh. Mengi wa IPP,

Leo agenda kuhusu Mengi itajadiliwa kwa kina katika kikao cha baadae. Ifahamike kuwa Vyombo vya habari vya Bwana Mengi vimekuwa vinalielezea jambo hili kwa uwazi na uhuru mkubwa kiasi cha umma kulielewa.

Ray: Chuchu Ndio Kila Kitu Kwangu, Johari na Mainda Tupa Kule

Posted: 21 Nov 2014 10:38 PM PST

Stori: Musa Mateja
LEGENDARY kwenye anga la sanaa Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa mara ya kwanza amefunguka kuwa mpenzi wake wa sasa, Chuchu Hans ndiye kila kitu na kilichobaki ni ndoa tu.

Akizungumza na paparazi wetu, Ray alisema licha ya kupitia katika changamoto nyingi za mapenzi lakini kwa Chuchu amefika na haoni tabu kujinadi kwa mtu yeyote juu ya penzi lake hilo.

“Chuchu ndiye kila kitu kwangu, tunaendana kwa kila kitu hivyo nitakaowaudhi kwa kumpenda yeye, wanisamehe,” alisema Ray.Ray kabla ya kuwa na Chuchu, kwa nyakati tofauti alikuwa akitajwa kushea penzi la mwigizaji Ruth Suka ‘Mainda’ na Blandina Chagula ‘Johari’.

Mchumba wa Agness Masogange Aibuka na Kusema Haya Kuhusu Kusalitiwa

Posted: 21 Nov 2014 10:36 PM PST

STORI: Musa Mateja
MCHUMBA wa Video Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ aitwaye Evance Kom juzikati alijikuta akivunja ukimya kwa kuweka wazi kuwa msichana huyo amemsaliti baada ya kuvunja makubaliano yao.
Akizungumza na gazeti hili Jumatatu hii, alisema hana tena mpango wa kuoana na Agnes kwani kitendo chake cha kuamua kuhamia Afrika Kusini kimeonyesha wazi hawawezi kuishi tena pamoja.Akisimulia, Evance alisema hapo awali walikubaliana kuwa pamoja kiasi kwamba hadi kufikia kumvalisha pete, wazazi wa pande zote mbili walikwishajua na kubariki uhusiano wao.

“Wakati anapanga mipango yake ya kuhamia Afrika Kusini, hakuwahi kuniambia hata mara moja, alikuja kuniambia eti tuhamie huko siku chache tu kabla hajaondoka, nisingeweza kuondoka na kwenda kuanza maisha mapya huko wakati hapa Bongo nina miradi yangu kibao,” alisema.

Alisema kutokana na kitendo hicho cha kuhamia huko, pia mchumba wake huyo alikuwa amejiingiza kwenye mambo yasiyofaa ambayo wazazi wake wasingeweza tena kumsapoti kama angehitaji kuendelea na nia yake ya kumuoa.

“Nilimpenda sana Agnes na yeye alinipenda lakini alichokiamua ni kizuri kwake, ila kwangu ni kama amenisaliti maana kajiingiza kwenye mambo yasiyofaa hivyo kwa sasa amebaki kama rafiki yangu wa kawaida tu,” alisema.

Taarifa za Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono Kulishwa Sumu

Posted: 21 Nov 2014 10:25 PM PST

 Nimrod Mkono amekoswakoswa kuuawa nchini Uingereza alikokuwa amekwenda kikazi. Aliwekewa sumu ambayo ilipaswa iharibu kabisa figo zake ndani ya saa 72. Uongozi wa bunge umethibitisha na ripoti ya madaktari wa London inaonesha hivyo. Mkono mwenyewe anasema alionywa kuwa usalama wake uko mashakani na akatakiwa asifikie katika hoteli ambayo ujumbe wa viongozi wa Tanzania utafikia. Mkono anasema alipofika London aliamua kwenda katika nyumba yake binafsi, lakini baadaye alianza kutoka jasho, kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu kwa saa 6. Ikumbukwe kuwa Mkono na kampuni yake ya Mkono & Advocates ndiyo iliyokuwa inatetea upande wa TANESCO na Serikali katika kesi dhidi ya IPTL. Inasemekana Mkono anatafutwa kuuawa kwa sababu inaonekana ana taarifa nyingi mno kuhusu sakata la IPTL na ESCROW, na serikali inamtuhumu kuwa yeye ndiye aliyevujisha nyaraka zote hadi umma wa watanzania kugundua kuwa zaidi ya bilioni 321 mali ya umma zimeibiwa katika sakata hilo.

Udaku Specially

unread,
Nov 23, 2014, 4:15:12 PM11/23/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Picha za Diamond Akimla Denda Zari the Boss Lady Zavuja Mitandaoni

Posted: 23 Nov 2014 03:59 AM PST

Duu Yameongelewa Mengi Wengine wakisema ni wapenzi wengine wakikataa na kusema ni Project ya mziki wanafanya pamoja ..Ila hii Picha inaelezea Yote ..Unachoona Ndio Hicho Kubali ama kataaa..
New Couple in Town !!
Wapi Team Wema???
Mupo Hapo

Al-Shabaab Wavamia Basi na Kuua Watu 28, Nairobi

Posted: 23 Nov 2014 02:47 AM PST

Takriban watu 28 wameuawa na watu wanaodaiwa kuwa wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab waliovamia basi la abiria jijini Nairobi, Kenya.

Tukio hilo limetokea alfajiri leo saa 11:30 kwenye eneo la Mandera.

Kamishna Msaidizi wa kaunti ya Mandera East, Elvis Korir alisema taarifa za awali zimedai kuwa wanamgambo hao takriban 100 waliisimamisha basi hiyo na kuamuru watu wote watoke nje.

Anadai kuwa abiria hao waliwekwa kwenye makundi mawili ya Wasomali na wasio wasomali. Alisema kundi la wasio wasomali walimiminiwa risasi.

Abiria 59 walikuwa wamepanda basi hilo.

Chanzo: Daily Nation

Jibu la Diamond la Kwanini Ametumia Tena Wazungu Kwenye Video Mpya ‘Ntampata Wapi’

Posted: 23 Nov 2014 02:46 AM PST

Baada ya Diamond kuachia video ya ‘Ntampata wapi’ iliyofanyika Afrika Kusini, amekutana tena na maswali aliyokutana nayo kipindi alipoachia video ya ‘Mdogo mdogo’, ya kwanini amewatumia zaidi wazungu kwenye video ya wimbo wake wenye ladha ya Kiafrika. 

Hili ndio jibu la Platnumz baada ya kuulizwa swali hilo kwenye kipindi cha Power Jamz kupitia East Africa Radio:

Kuna kitu kimoja, waache ubaguzi inategemea na script ya nyimbo inavyozungumza, script inataka kitu gani, script yangu ya mdogo mdogo ilikuwa inazungumza kwamba mapenzi hayachagui, ndio maana kulikuwa na familia ya kizungu mimi familia ya kiafrika, mimi namtaka demu wa kizungu lakini wazazi wake hawataki, kwahiyo ndo maana mwisho tukaandika mapenzi hayachagui”.

Na naamini hicho kitu ndo kilisababisha kufanya hata Marekani ikashinda tuzo, video ya Aye haikushinda ikashinda video ya Mdogo mdogo kama video ya Afrika kwasbaabu concept yenyewe ilikuwa inazungumza vizuri, wazungu wenyewe wameona kama aah hii kweli lakini tuache maswala ya kibaguzi”.

Breaking: JAJA Ajiondoa Rasmi Yanga, EMERSON Achukua Nafasi Yake

Posted: 23 Nov 2014 01:40 AM PST

MSHAMBULIAJI Genilson Santana Santos ‘Jaja’ amejiondoa Yanga SC
akiwa likizo nchini mwao, Brazil na sasa nafasi yake itazibwa na
kiungo mkabaji, Emerson Oliveira Neves Roque, Jaja amesema ana matatizo ya kifamilia yanayomzuia kurejea
Tanzania kufanya kazi.
Emerson mwenye umri wa miaka 24 mzaliwa wa Rio de Janeiro,
anakuja Yanga SC akitokea klabu ya Bonsucesso ya mjini humo, ambayo imewahi kucheza Ligi ya Serie B
mara mbili, ingawa kwa sasa inacheza ligi ya jimbo la Rio.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuwasili Dar es Salaam Jumanne kwa ajili
ya kufanyiwa majaribio na akifuzu atafanyiwa vipimo vya afya, kabla
ya kusajiliwa. Wazi mchezaji huyo ana nafasi ya kusajiliwa Yanga SC
kwa kuwa analetwa na kocha Maximo.

Kucha za Bandia zile za Kubandika na Gundi Samsababishia Mauti Bibi Harusi

Posted: 23 Nov 2014 01:24 AM PST


“Sijui walitumia gundi ya aina gani
kumbandikia kucha mwanangu, mpaka sasa sielewi, mtoto mwenyewe ndiyo huyo huyo mmoja wa kike niliyekuwa nikimtegemea na ndiyo kwanza ndoa yake bado change kabisa hata mwezi mmoja haina, huu ni mtihani mkubwa kwangu na kwa mumewe ambaye wamefunga naye ndoa wiki tatu zilizopita, inauma sana lakini
tunamwachia Mungu.”

Ni maneno ya mama mzazi wa Sophia Komba aliyefariki dunia hivi karibuni jijini Dar es Salaam, baada ya kupata kidonda kwenye kidole chake cha mkono wa kushoto alipokuwa akibandua kucha za bandia alizobandikwa siku ya harusi yake na kusababisha apatwe na tetenasi.
Sophia hadi kifo kinamkuta alikuwa na umri wa miaka 28, Oktoba 15 alifunga ndoa na Richard Mmary katika harusi ya aina yake iliyofanyika jijini Dar es
Salaam.
Wakisimulia namna walivyomuuguza Sophia kwa takriban wiki moja na
nusu, mume wa marehemu anasema
wiki moja baada ya sherehe ya harusi yao, Sophia aliamua kwenda tena salon kwa ajili ya kutengeneza nywele na kutoa kucha alizobandikwa siku ya harusi yao.
“Ilikuwa siku ya Jumamosi jioni,
Sophia aliniaga anaenda saluni, alirudi baada ya saa mbili kupita lakini alikuwa akilalamika kuwa kidole kinamuuma sana, nikamuuliza amefanya nini akanijibu kuwa alikuwa anabandua kucha, lakini bahati mbaya kucha moja inaonekana ilibandikwa vibaya walipokuwa wanaibandua ilibanduka na ngozi ya pembeni ya kidole na ikamuachia kidonda.
“Sikujali sana nikajua ni kidonda cha
kawaida tu, nikaenda kwenye duka la dawa nikamnunulia spiriti
nikamsafisha lile eneo, lakini
kilichonishangaza alikuwa akilalamikia maumivu makali,” anasema.
Mama yake Sophia, Victoria Haule
anasema kuwa anaamini kuwa kifo cha mwanaye kimetokana na kucha bandia ambayo ilimsababishia apatwe na
tetenasi.
“Tulipoona maumivu yanamzidia,
tulimpeleka Hospitali ya Sinza, daktari alipomfanyia vipimo alitutaka tumpeleke Hospitali ya Mwananyamala kwa matibabu zaidi, kwa kuwa alibaini kuwa Sophia ana tetenasi iliyosababishwa na kile kidonda.
Binafsi niliamini kucha ile ndiyo
tatizo, kwa kuwa ilifikia hatua mkono
mzima ukawa umevimba na
kubadirika rangi na kuwa mweusi sana kama damu imevilia,” anasimulia mama yake Sophia.
Kwa maelezo ya ndugu hao wa
marehemu, Sophia alifariki dunia
akiwa anapatiwa matibabu na kwa
mujibu wa daktari kifo chake
kilisababishwa na tetenasi.
Mabibi harusi wengi hivi sasa na hata wanawake kwa wasichana
wanapendelea sana kubandika kucha bandia wakilenga kuboresha
mwonekano wa vidole vyao. Wengi
hupenda kuwa na kucha ndefu ambazo huzipaka rangi na hivyo kuvutia pindi mtu azionapo.

Sakata la Mtoto Aliye Teswa na House Girl, Waajiri Tujifunze Kitu Muhimu Hapa

Posted: 23 Nov 2014 12:50 AM PST

Dah kwa alieoona clip hii ataamini kuwa baadhi ya wanawake wana roho za kikatili. Na sijui huyo msichana ningemfanya nn katika nafasi ya yule baba. Maana.. Na vile naskia habari tofauti wengine wanasema mtoto ameshaaga dunia , wengine wanasema yupo mahututi amepata tatizo la uti wa mgongo. Mungu asimame tu!

Yote sawa, hiki sio kigezo cha kunyanyasa wafanyakazi kwa sababu sio wote wenye roho katili hivi. Wengine wanaanza ukatili baada ya kukatiliwa na mabosi wao. Kuishi vizuri na hawa watu ni muhimu sana. Wao pia ni binadamu.
Ila pia haya ndio maisha ya watoto wengi wanaolelewa na kina mama wa kambo, ni basi tu wengi wao hawajakamatwa na cameras.
Wanaume wanaopenda kuzaa zaa , mtu unakuta anazaa pengine na kuoa pengine, mnaweka damu zenu zisizo na hatia katika ukatili huu. Istoshe suala la uzazi wa mpango limerahisishwa sana.
Ni ushauri tu kwa wanaume, waoe walipozalisha au wazae BAADA TU ya ndoa. Sababu hii ni hulka ya mwanamke ambayo haiwez badilika, hata akupendeje huyo mwanamke, atakunyanyasia mwanao hivi.
Na wazazi waliooana ni vema kudumisha familia kakamavu , lasivyo kutengana kwa Baba na mama huchangia hali.. Hii kwa kiasi kikubwa.
Nia yangu kuu ni , tujue kuwa maamuzi yetu ya sasa yanaashiria kitu mbeleni katika maisha yetu.Tusiwe wachoyo kwa kujifikiria tu na furaha za nafsi zetu, tujali hata wa pembeni yetu pamoja na damu zetu. Tunaweza sambaza upendo kwa kutenda kwa busara leo hii na kila mtu akaishi kwa.furaha na amani.

By Leah-Buzuka Derefa

Maneno ya Meneja wa Wema Sepetu Kadinda Kuhusu Kumwachanisha na Diamond na Wema

Posted: 23 Nov 2014 12:22 AM PST

Kama macho yako hayakosi Magazeti ya kila siku au kusoma mitandao mbalimbali ni lazima utakua umekutana na stori kwamba Wema Sepetu na Diamond Platnumz wameachana.
Diamond Platnumz alihojiwa kwenye XXL ya CloudsFM November 21 2014 lakini hakuweka wazi kabisa nini kinaendelea lakini maelezo yake yanaweza yakawa na ishara ya jibu linakoelekea.

Moja kati ya alivyovisema ni kwamba hata yeye alishangaa kuhusu ile zawadi ya gari aina ya BMW aliyozawadiwa Wema kwenye birthday yake huku meneja wake Martin akikaririwa na vyombo vya habari kwamba ni marafiki walijichanga kumnunulia Wema.

Baada ya hayo kuna baadhi ya stori zimekua zikitambaa kwamba Martin Kadinda ndio amehusika kuwaachanisha Diamond na Wema Sepetu ambapo aliamua kujibu kwa kuandika hivi kwenye instagram >>> ‘Siwezagi kujibizana.. Ila i gat people who can do that…. Namleta kwenu bingwa wa kutusi watu… Mimi nimemwachanisha wema na chibu ahahahahahaa ahahhahahaha ahahahahaha walaaahi naona raha.. We Nasri that powerful couple ambayo haijawahi kutokea tz na haitakuja kutokea iachanishwe na mimi fundi makoti?? Team kadinda mpeni what he deserve…..’




Ripoti ya CAG Yavuja, Baadhi ya Kurasa Zinazodaiwa Kuchomolewa Zawekwa Wazi

Posted: 23 Nov 2014 12:18 AM PST

Ripoti ya CAG YavujaBaadhi ya kurasa zinazodaiwa kuchomolewa zawekwa wazi na ripoti nzima yadaiwa itawekwa hewani endapo kutatokea kuchakachua

Kimsingi, ripoti nzima ipo na itawekwa hewani endapo michezo inayochezwa itaendelea!

Nimesikitishwa na taarifa za kuanza kunyofolewa kurasa za ripoti hii; bahati nzuri kuna watu wanayo original copy na imeshasambaa sana hivyo ni vema wahusika wakaacha wabunge waifanye kazi yao kwa kadiri inavyostahili.

Hatungependa kuingilia sana lakini tunaona kama tunalazimishwa kufanya hivyo.

DOKEZO:

Hizi chini ni baadhi ya kurasa zinazodaiwa kunyofolewa...


Source:Jamii Forums

Udaku Specially

unread,
Nov 24, 2014, 4:48:10 PM11/24/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


U Heard ya leo Kuhusu Nay wa Mitego na Kala Jeremiah Kuchuniana Baada ya Nay Kumdis Kala Kwenye Wimbo

Posted: 24 Nov 2014 08:25 AM PST

Kama umepitwa na U Heard kwenye XXL ya leo nimekuwekea hapa, zimesikika taarifa kuhusu Kala Jeremiah na Ney wa Mitego.
Baada ya tetesi nyingi kuenea mtaani kuhusu wasanii wawili ambao walikuwa hawaongei karibu miezi mitano kisa kikidaiwa ni mambo ya nyimbo zao.
Mwezi wa sita msanii Kala Jeremiah aliachia nyimbo ya ‘Simu ya Mwisho’ alichomshirikisha Ney wa Mitego, haukupita muda mrefu Ney akaaichia Mr. Ney ambapo ndani yake alimtaja Kala Jeremiah kuwa kapotea kwenye game na huo ukawa mwisho wa wasanii hao kuwasiliana kama ilivyokuwa zamani.
Wakali hawa wamekutana Ubungo kwenye studio ya mtengeneza Video, Pablo na maongezi yao yalikuwa poa, kama watu ambao hawana tofauti yoyote.
U Heard nimekuwekea hapa, unaweza kuisikiliza kwa kubonyeza play.


Download Wimbo Mpya wa Lady Jay Dee Feat. Dabo -Forever

Posted: 24 Nov 2014 08:11 AM PST

Download Wimbo Mpya wa Lady Jay Dee Feat. Dabo -Forever

Lundenga Awaka Kisa Kuulizwa Kuhusu Sitti Mtemvu

Posted: 24 Nov 2014 07:49 AM PST

Stori: Musa Mateja
MKURUGENZI wa Lino International Agency ambao ndiyo waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga amewaka kinomanoma baada ya kuulizwa habari za mrembo wake aliyejivua taji hivi karibuni, Sitti Mtemvu

Lundenga alibwatuka maneno makali baada ya paparazi wetu kumuuliza juu ya uwepo wa taarifa kwamba shindano hilo linaweza kufungiwa kutokana na kashfa mbalimbali zinazolitafuna sambamba na ufafanuzi wa zawadi ambayo alipewa Sitti kama anaweza kuirejesha kwa mrembo namba mbili aliyechukua nafasi yake.

“Sikiliza nyinyi nawaheshimu sana sababu najua mpo makini, tusivunjiane heshima hizo habari zisizokuwa na kichwa wala miguu waachieni wanaokurupuka kuandika mambo ya uongo, wapuuzi sana wale,” alisema Lundenga na kukata simu na hata alipopigiwa tena, hakupokea.

Pinda - Mjadala Escrow Umeongezwa Chumvi, Watanzania Msiamini Mambo ya Uzushi

Posted: 24 Nov 2014 07:45 AM PST

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema taarifa nyingi za mjadala wa akaunti ya Escrow iliyofunguliwa kutokana na mgogoro wa malipo ya gharama za umeme kati ya kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ambao unaendelea bungeni, umeongezwa chumvi na wakati ukifika Watanzania watatolewa taarifa kamili.

Kauli hiyo ya Pinda aliitoa kanisa kuu la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika wakati wa kumsimika Dk Jackson Chilongani kuwa Askofu wa Sita wa dayosisi hiyo.

Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Jacob Chimeledya aliitaka Serikali kutoa taarifa juu ya akaunti ya Escrow ili wananchi wajue kilichotokea ili ijulikane ukweli upi na uvumi upi kwani iko hatari ya kutengeneza taifa lenye kuamini uvumi.

Dk Chimeledya alisema Watanzania sasa wanaishi kwenye hali ya sintofahamu kwani hawajui yupi anasema ukweli na yupi ni `mzushi’. Alisema ni lazima Serikali itoe maelezo kwa wananchi juu ya kashfa hiyo ili wajue kilichotokea kwani ipo hatari ya kutengeneza taifa linaloishi kwa kuamini uvumi.

“Hatutakiwi kuishi kwenye taifa linaloamini uvumi… taifa halitapiga hatua kwa taarifa za kusikia tu bila kujua ukweli uko wapi, nini kimetokea na hatua gani imechukuliwa,” alisema

Aibu: Msanii wa Bongo Movies Afumwa Makaburini Akivunja Nazi ili awe Maarufu Kama Wema Sepetu

Posted: 24 Nov 2014 07:33 AM PST

Ulozi! Chipukizi sinema za Kibongo, Fatuma Ayubu ‘Fetty’ amenaswa makaburini akiwanga katika kile kinachodaiwa kuwa ni kutekeleza masharti ya ‘sangoma’ ili ajipatie umaarufu na kuwafikia mastaa kama Wema Isaac Sepetu, Jacqueline Wolper Massawe na Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Makaburi ya Ufi yaliyopo maeneo ya Ubungo-Kisiwani jijini Dar, mishale ya saa nne usiku.


Habari zilidai kwamba msanii huyo alifumwa akivunja nazi na kuzungumza maneno yasiyoeleweka.
Awali, ilidaiwa kwamba, Fetty ambaye anaonekana kwenye Filamu ya House of Death akiwa na mwigizaji Kulwa Kikumba ’Dude’ alitinga kwenye makaburi hayo akiwa ameshika kimfuko huku akiangaza huku na huku kisha akatoa nazi na kuivunja huku akinuiza maneno bila kujua kuna mtu alikuwa akimpiga picha.

Ijumaa Wikienda lilipomtafuta Fetty na kumuuliza juu ya madai hayo, alianza kujikanyaga kabla ya kufunguka kuwa hapendi mambo ya kishirikina ila alilazimika kufanya hivyo kutokana na masharti aliyopewa na mganga wake kutokana na matatizo yake ya kimaisha yanayomsumbua pamoja na ndoto yake ya kuwa msanii mkubwa.

Pinda, Werema na Muhongo wataka zigo la Escrow abebeshwe Kikwete!

Posted: 23 Nov 2014 09:51 PM PST

Dodoma kumekucha. Naomba kwa ufupi niwafahamishe kinachojiri maeneo haya (nimepiga kambi huku).

MOSI:
Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa anataka PM Pinda atoke kwa sababu mbili, moja ili njia ya kupata Urais iwe nyeupe lakini pili ili asiwe PM peke yake aliyewahi kujiuzulu kwa tuhuma za rushwa. Watu wake Edward wanahangaika sana kushawishi watu ili azma hii itimie.

PILI:
Membe naye anataka PM ang'oke kwa sababu kuu mbili, moja ili njia ya Urais iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM japo kwa muda tu ili nyota ing'are zaidi.

TATU:
Wassira naye anatakaPinda aanguke ili njia iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM.
Mwandosya naye anataka PM adondoke kwa matumaini ya kupata uPM kutokana na utu uzima.

Sitta naye vivyo hivyo.

NNE:
Mawaziri walioondolewa huko nyuma wakiongozwa na Kagasheki, Nchimbi na Maige nao wanaomba Serikali idondoke kwa sababu wanaamini Pinda aliwatosa ili apone yeye na sasa wanataka na yeye awajibike kwa udhaifu wake. Yupo mtu kama Mwigulu ambaye anautaka Uwaziri kamili kwa udi na uvumba na anataka Serikali ianguke ili Baraza la Mawaziri lisukwe upya awe Waziri kamili.

Kambi za Urais za wazee zimeungana kutaka Pinda ang'oke!

TANO:
Kwa upande mwingine hii ni vita ya watu wa Mara: Maswi, Muhongo, Werema na Mkono. 

Upande mwingine ni vita ya baina ya vizazi; kizazi cha vijana na kizazi cha wazee.

Tazama Vijana walioshikilia bango suala hili ni wabunge vijana: Zitto, Kafulila, Filikunjombe, Serukamba, Mpina, Bulaya, Kigwangalla n.k.

Wanaotetea ni watu wazima: Pinda, Muhongo, Werema na wengine.

Lakini pia kwa Upande mwingine ni vita ya pesa: Kila upande umekula na ujanja ni kuwahi kupaka matope wengine!

SITA:
Kamati ya PAC imeandika ripoti nzito zaidi ya ripoti ya CAG ambayo ni laini mno (nimebahatika kuziona walau zote mbili). PAC, chini ya Zitto na Filikunjombe wanaweza kuwa wamefanikisha kufanya ripoti yao iwe vizuri hivyo kwa sababu wamewahoji watu na kupata taarifa za ziada (ambazo zitaibua mjadala mzito sana Bungeni).

SABA:
Pinda anapigana kufa na kupona ili apone. Pinda akianguka hapa Urais ndio kwisha. Hata hivyo, Pinda hata asipotoka uPM atakuwa tayari amechafuka na udhaifu wake umebainika. Ijapokuwa Wabunge wanaweza kumponya tu Pinda kwa sababu ya kumsaidia Kikwete lakini tayari ana doa!

Hata hivyo, katika harakati za kupona Pinda, Werema na Muhongo wamekuwa wanawaambia wabunge kwamba kulikuwa na agizo la Rais la pesa kulipwa. Yaani Pinda yuko tayari kumuingiza Rais kwenye tope kulinda vyeo vyao!

Kikwete inabidi afanye maamuzi ya Kiurais, watu aliowaamini hawana hiyana kumtosa. Akimaliza Urais ndio hatari zaidi (mtakumbuka kauli yangu 2016/2017)

Wanaume Tunarogwa Sana na Hawa Wanawake Zetu

Posted: 23 Nov 2014 09:42 PM PST

Katika Uchunguzi Wangu nimegundua Wateja wengi wa waganga wa Kienyeji ni wanawake ,hii inatoka na kuwa ushindani wa namba umekuwa mkubwa sana matokeo yake wakina dada na wakina mama wamemua kutafuta plan B nayo si nyingine ni kutuchawia, tunarogwa sana,  tunalishwa vitu vya ajabu.

Wateja wakubwa wa waganga ni hawa wanawake unadhani wanafuata nini huko kwa Waganga?

Ni aibu India na Kenya Kuipiku Tanzania kwa Uuzaji Madini ya Tanzanite yanayopatikana Tanzania Pekee

Posted: 23 Nov 2014 09:32 PM PST

Taarifa kwamba nchi za Kenya na India zimeipita kwa mbali Tanzania kwa kusafirisha madini ya Tanzanite yanayopatikana hapa nchini pekee na kuyauza katika soko la dunia ni jambo ambalo siyo rahisi kuliamini.

Nasema siyo rahisi kuamini kwa sababu haingii akilini hata kidogo, mtu ambaye halimi mahindi anaibuka kinara wa kuuza sokoni mahindi yako anayoyaiba shambani kwako.

Ni heri kama angekuwa anakuja kununua kwa njia ya kawaida na wewe ukanufaika.

Nilimsoma kwa makini Kamishna wa Madini katika Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja hivi karibuni kupitia baadhi ya magazeti nchini akisema kwamba kwa mwaka jana, Tanzania haikufikia hata nusu ya Kenya kwa mauzo ya madini hayo ya vito.

Mwaka jana pekee, Kenya ilisafirisha na kuuza nje ya nchi Tanzanite yenye thamani ya zaidi ya Dola za Marekani 100 milioni (Sh173 bilioni), dhidi ya Dola 38 milioni (Sh45.5 bilioni), zilizouzwa na Tanzania.

Katika kipindi hicho cha mwaka jana, India iliuza Tanzanite zenye thamani ya zaidi ya Dola 300 milioni za Marekani(Sh509 bilioni) kiasi cha baadhi ya wanunuzi wakubwa, hasa kutoka Marekani kujiuliza iwapo madini hayo yanachimbwa India.

Mmoja wa wanunuzi wakubwa wa madini ya vito kutoka Marekani, aliwahi kuwauliza viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini iwapo kuna migodi ya Tanzanite India kwa sababu akifika huko hupata Tanzanite bora na zenye ukubwa kuliko anayopata Tanzania.

Taarifa zinaeleza kuwa, zaidi ya asilimia 80 ya Tanzanite inayopatikana Mirerani, Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, huuzwa kwa njia za panya nje ya nchi na kwamba Serikali imeanza kuchukua hatua.

Kama nilivyosema awali, hili ni jambo la kushangaza sana. Ninajiuliza; hivi haya madini nani anayeyatorosha kwenda nchi za nje? Ni wazi kuwa watu wachache waliopewa jukumu la kusimamia sekta ya madini, wamekuwa wakishirikiana na watu wa nje kutorosha madini hayo.

Tumejua wizi wa madini haya kwa sababu tu yanapatikana pekee Tanzania. Tujiulize wizi huu wa madini yetu ukoje katika madini mengine ambayo pia yanapatikana katika nchi nyingine?

Kwa hakika, raslimali za nchi hii zinaliwa na watu wengine, huku Watanzania wakibaki mikono mitupu.

Mwigulu Nchemba Acharuka Asema Walio iba Fedha za Escrow Wakamatwe na Kufilisiwa Mali zao

Posted: 23 Nov 2014 09:24 PM PST

Mwigulu Nchemba alitoa msimamo mkali kuhusu sakata hilo la escrow na kwamba ametaka hatua zichukuliwe kwa wahusika wote.

Katika kikao hicho inaelezwa kwamba Nchemba alionyesha msimamo wake waziwazi kuwa sakata hilo ni hujuma  na kwamba haiwezekani walioiba fedha hizo wakaachiwa tu hivihivi.

Ndani ya kikao hicho imeelezwa kuwa Mwigulu alijitokeza na kusema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ameshamaliza utata hivyo, mali zote, fedha zote za IPTL zikamatwe na wahusika wote wakamatwe.

Alisema haiwezekani watu wakawajibika tu kwa kujiuzulu kwa kuwa huko ni kutoa tu likizo mtu akale mabilioni yake, hivyo wachukuliwe hatua ipasavyo na kufilisiwa.

“CAG ameshasema pesa zile zilikuwa mali ya umma, sasa zikamatwe zote na wahusika wote wakamatwe,” alisema Mwigulu.

Chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa Mwigulu alienda mbali zaidi na kusema hata ambao walishastaafu na wamehusika kulihujumu taifa wakamatwe na akaunti zao zikamatwe, zifilisiwe na fedha zirudishwe kwa wananchi.

Pia aliagiza mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambaye anatuhumiwa kuchota Sh1.6 bilioni za akaunti hiyo afukuzwe kazi, akamatwe na akaunti zake za fedha zifilisiwe ili fedha irudi serikalini.

Habari za uhakika kutoka kikao hicho zinaeleza kuwa Mwigulu aliongea kwa sauti ya mamlaka mbele ya Waziri Mkuu na kusema kuwa kujiuzulu siyo adhabu stahiki kwa wizi mkubwa kama huo.

Mwigulu alisema: “Tazama wanafunzi, watoto wa maskini zaidi ya elfu 40 wamekosa mikopo, madawa hospitalini hakuna, maskini wanakufa, watu wasio na hatia wanafungwa kwa kukosa michango ya maabara, walimu wanadai fedha zao, wazabuni wanauziwa nyumba zao na benki huku wakiidai Serikali kwa huduma walizotoa, leo wezi tuwape adhabu ya kujiuzulu? Tuwape likizo ya kwenda kutumia fedha walizo waibia maskini?”

Kwa mtumishi wa TRA aliyekula fedha za IPTL zaidi ya 1.6 bilioni Mwigulu akatoa agizo:

Nimemwagiza Kamishna wa Kodi amfukuze kazi yule mtumishi wa TRA iliyoko chini ya wizara yangu na afilisiwe, pia mitambo na kodi vikamatwe na wahusika wakamatwe.

Hatuwezi kuendeleza mazoea ya kufunga maskini na kuwapa likizo wezi wakatumie fedha. Walio serikalini na walioko kwenye siasa wakamatwe na tuwafilisi fedha irudi serikalini,” Mwigulu alisisitiza.

Udaku Specially

unread,
Nov 25, 2014, 4:45:08 PM11/25/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Bunge haliwezi kupewa zuio na Mahakama, Taarifa ya PAC Itawasilishwa Kwa Mujibu wa Ratiba

Posted: 25 Nov 2014 07:39 AM PST

'Bunge haliwezi kupewa zuio wakati mkutano ukiendelea. Injunction itoke au isitoke Taarifa ya PAC itaingia. Majaji wasome Katiba na Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge' Zitto

Mahakama Kuu imesimamisha mjadala wa Ripoti ya Escrow kujadiliwa Bungeni

Posted: 25 Nov 2014 07:25 AM PST

Nimepata taarifa muda huu kutoka kwa mtu aliyeko Mahakama Kuu kuwa kutokana na taarifa iliyokuwa inaelezwa kuwa jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu watasikiliza kesi iliyofunguliwa na IPTL na PAP kuzuia bunge kujadili suala la Escrow.

Imeamriwa na Mahakama Kuu chini ya jopo la majaji watatu kuwa wamesimamisha mjadala wa Ripoti ya Escrow hadi hoja za msingi zitakapo fanyiwa kazi.

Jeshi la Kenya Ladai Wameua Al shabaab 100 Baada ya Shambulio liliouwa Wakenya 28

Posted: 25 Nov 2014 05:08 AM PST

Makamo wa rais wa Kenya, William Ruto, anasema kuwa askari wa usalama wa Kenya wamewaandama wapiganaji wa al-Shabaab hadi kwenye kambi yao nchini Somalia, baada ya shambulio dhidi ya basi kaskazini-mashariki mwa Kenya hapo jana ambapo raia 28 waliuliwa.
Bwana Ruto alisema wapiganaji zaidi ya 100 waliuliwa katika operesheni mbili tofauti.
Alisema kambi ya al-Shabaab iliangamizwa.
Habari hizo hazikuthibitishwa na upande wa pili.
Gavana wa Mandera - ambako shambulio la jana lilitokea - amelaumu vikosi vya usalama kwa kushindwa kuwalinda raia.
Alisema polisi kawaida wanashindwa kufanya uchunguzi kamili baada ya mashambulio.

Mwanamke yeyote Akikupa Mara Moja, Hata Akiolewa Ukimwomba Tena Atakupa Bila Shida

Posted: 25 Nov 2014 04:49 AM PST

Aaahh... nilifuatilia hili hadi nimepata almost 75% wanasema kama ukishakuwa na uhusiano
na mwanamke kabla ya kuolewa/ akiwa ndani ya ndoa yaani mmekuwa mnamegana, na kuachana kwa sababu nzuri tu, labda kaolewa kahamia mbali, au kahamishwa kazi then akaja olewa au ulishalala na mwana mke mara moja na hamjagombana siku yeyote ukimwomba hawezi kukunyima, so wanaume watalaam wa mapenzi ni vigumu kugombana na wanawake wanajua siku moja wataonana na kupewa as usual, awe ameolewa au single ili mradi upate SIKU MOJA then siku zijazo hakuna kutongoza , just make a call na kupanga time utapewa......

By Chapa Nalo Jr

Haya Ndio Yanayoendelea Kuhusu Yule Binti Mfanyakazi wa Ndani Aliyeonekana Akimtesa Mtoto

Posted: 25 Nov 2014 04:35 AM PST

Polisi wamebadilisha mashtaka ya mfanyikazi wa nyumbani aliyenaswa kwa kamera akimpiga na kumtendea unyama mtoto wa mwaka mmoja na nusu, kutoka kwa kosa la kutesa na sasa anakabiliwa na kosa la jaribio la mauaji.
Video hiyo iliwaudhi watu wengi sana kwenye mitandao ya kijamii ila babake mtoto huyo alisema walisambaza video hiyo ili kuwatahadharisha wazazi wenegine.
Mfanyakazi huyo wa nyumbani Jolly Tumuhirwe, alikuwa amezuiliwa katika gereza la Luzira na mahakama ya Nakawa kwa kosa la kutesa chini ya kifungo cha 41 kwenye katiba kinachoongelea dhidi ya mateso.

Mwanamke huyo sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 8 Disemba.
Hata hivyo, msemaji wa polisi Bwana Fred Enanga, amesema "shtaka dhidi ya mwanamke huyo lilibadilishwa baada ya kupitiwa mwendesha mkuu wa mashitaka.
Tumuhirwe alikubali kosa la kumpiga mtoto huyo kwa kurunzi, tuki olililonaswa kwa kamara ya CCTV. Polisi walimfanyia Tumuhirwe uchunguzi wa kiakili na kubaini kuwa ana akili timamu.
Afisaa mkuu wa polisi Fred Enaga, amewaonya waajiri kuchunguza mbinu zinazotumika kuwachagua wasichana wa kazi, kwa sababu matendo kama haya yanaweza kutokana na matatizo ya kisaikologia.

Waziri wa Jinsia, Kazi na maendeleo ya jamii Bi Mary Karooro Okurut alipongeza juhudi za wazazi wa mtoto huyo Arnella "kutokana na kitendo hicho kwa mtoto. Ingekuwa mtu mwingine angemuua mischana huyo wa kazi lakini alifuata sheria. Pia tunapeleka marekebisho katika katiba kuhusu maslai ya watoto bungeni kuimarisha sheria zinazowajali watoto," alisema waziri huyo.
Polisi wamesema kuwa nia ya shambulio hilo haijatambulika na pia msichana huyo amefanyia kazi familia hiyo kwa siku 26 pekee. Wazazi wamesema kuwa mtoto huyo ametolewa hosipitalini na hali yake ya afya inaimarika.

Kulingana na msemaji wa polisi Fred Enaga, kesi hiyo iliripotiwa na Baba ya mtoto Erick Kamanzi mnamo tarehe 13 Novemba katika kituo cha polisi cha Kiwatule baada ya kuona video hio.
Kesi hiyo ilipelekwa kwa kitengo cha polisi cha Kiira. Baada ya uchunguzi, msichana huyo wa kazi alihukumiwa na shataka la mateso katika mahakama ya Nakawa na kuzuuliwa katika gereza la Luzira.

Bwana Enaga alisema Bi Tumuhirwe alishtakiwa chini ya kifungo cha tatu kwenye katika kinacholinda maslahi ya watoto. Kifungo hicho kinajumuisha mashataka kama ya kutesa inayopeana uwezekano wa kumfunga mtu hadi miaka 15 gerezani.
Hata hivyo, Bwana Enaga anashauriana na mkurugegenzi wa pande za mashtaka kurebisha hukumu hilo kuwa kifungu cha maisha.

Naombeni Ushauri Wenu, Mpenzi Wangu Amekutwa na Maambukizi ya Ukimwi

Posted: 25 Nov 2014 04:24 AM PST

Jamani nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi na mdada mmoja hivi takribani ni miaka 3 sasa.

Katika mahusiano yetu tumekuwa tukipendana sana na hatma ya yote lengo letu lilikuwa ni kuishi wawili kama mume na mke.

Huyu mpenzi wangu tumekuwa tukiishi mbali mbali kutokana na wote wawili kuwa na majukumu tofauti ya kiutumishi.
Hapo mwanzo nilipoanza nae tulipima afya zetu yaani hatukuwa na maambukizi ya vvu.

Kiukweli tokea hapo tulijihusisha na mapenzi kwa uaminifu kila upande. Nimekuwa nikimuamini sana na yeye pia kuniamini. Mimi mwaka huu nilikuwa nimepanga tufunge ndoa mwezi wa 12. Mimi naishi mwanza kikazi ila yeye anaishi dodoma.

Tokea mwanzo wa mahusiano yetu sijawahi kutumia kinga ninapokutana na yeye na nimekaa naye kwangu mara nyingi sana pindi anapokuwa na likizo.

Mwezi uliopita amekuja kwangu nikawa nimekaa nae kama wiki mbili hivi akawa amepata homa tu ya kawaida.

Ikabidi nimpeleke hospitali kupata matibabu,tulivyoenda hospitali nikamshauri ebu leo tucheki bas afya zetu? Kwani ni muda sasa hatujacheck vvu.

Alikubali tukawa tumeenda kupima,majibu yaliyotoka ni kwamba yeye ana maambukizi ya vvu na kwa upande wangu sijaonekana na maambukizi.

Kiukweli hiki kitu kimeniumiza sana na hapa nilipo sijajua hatma ya maisha yangu,na daktari alichoniambia ni kwamba mimi damu yangu sio rahisi kupokea maambukizi ya vvu kutokana na group langu la damu na lake.

Hivyo amenishauri niendelee kupima kila baada ya miezi mitatu ili kuwa na uhakika zaidi.

Kitu kinachoniumiza na kunisumbua kichwa zaidi ni kwamba huyu mchumba wangu analia sana na anasema kutengana na mimi ni bora yeye afe tu kuliko kukaa mbali na mimi.

Na kingine ni kwamba,anadai kutokana na upendo wangu juu yake anataka anizalie mtoto ili aniachie zawadi hata yeye akifa.

Kiukweli hapa nilipo sijitambui afya yangu na kushiriki tena tendo na yeye naogopa.

NIFANYAJE Ili kumfurahisha? nikubali kuzaa nae? Nifanyaje 

Wanaume wa Dar mnaongoza kuvunja mahusiano yetu sisi tulio mikoani

Posted: 25 Nov 2014 04:21 AM PST

Jamani wanaume mliopo Dar es salaam tunaomba mtuhurumie sisi tulio mikoani, kwani ukiwa na mpenzi wako akikuaga anaenda Dar kusoma au kwa ndugu yake na akikaa angalau mwaka mmoja ujue akirudi sio wako tena mambo yanabadilika kabisa ..Maringo mengi na dharau juuu

Nashindwa kuelewa sijui mnawapa kitu gani wapenzi wetu wakija huko dar?

Mabibi na Mabwana ile single mpya ya Waje na Diamond ndio hii imetoka

Posted: 25 Nov 2014 03:44 AM PST

Ile single mpya ya msanii wa Nigeria Waje na Diamond Platnumz ‘Coco Baby’ iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu sasa imetoka nakukaribisha uisikilize hapa

Dully Sykes Ajitetea Kuhusu Wimbo wa 'Matusi' Aliyoutoa Hivi Karibuni

Posted: 25 Nov 2014 03:06 AM PST

Siku chache baada ya wimbo wake wa Thats The Way uliojaa matusi yasiyoweza kuandikika gazetini kuanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao , msanii wa kitambo wa muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amefunguka kuwa halikuwa kusudio lake kuachia wimbo huo bali ulivuja kwa bahati mbaya mitandaoni.

Akipiga stori na Showbiz juzikati, Dully alisema kuwa wimbo huo aliomshirikisha mwanadada Maunda Zorro, aliurekodi miaka nane iliyopita kwenye studio yake ya Dhahabu Records na hakupanga kuutoa lakini kwa bahati mbaya ukavuja na kuingia mitandaoni.

“Siyo mpya, ni wa kitambo sana, nilirekodi miaka nane iliyopita nashangaa kwa nini watu wanafikiri ni mpya,” alisema Dully lakini alipoulizwa hata kama ni wa zamani kwa nini alirekodi wimbo wenye maneno ya kuhamasisha ngono, hakuwa na majibu.

Licha ya utetezi wake huo, wimbo huo unaonekana kuwa mpya kwani sauti ya Dully inafanana na ya kwenye nyimbo zake mpya za hivi karibuni.

Zitto: Tumependekeza Kumvua Ujaji Mh. Werema

Posted: 25 Nov 2014 03:03 AM PST

Akihojiwa na mwandishi wa Tanzania Daima, mh. Zitto amesema PAC IMEPENDEKEZA

1. Kuanza mchakato wa kumvua UJAJI MH. WEREMA

2. Kumfikisha mahakamani

3. Wote waliohusika kuwajibishwa kulipa na kisha kupelekwa mahakamani.

Mh. Zitto amedai hii haiwezi kuisha kama EPA,lazima wahusika wafike mbele ya sheria.

Issue ya Madawa ya Kulevya, Chonji Hali Tete

Posted: 25 Nov 2014 03:01 AM PST

HALI tete, siku chache baada ya mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Muharani Mohammed Abdallah, maarufu kama Chonji kukamatwa na kutupwa gerezani kwa tuhuma za kukamatwa na dawa kulevya, sasa mali zake zimeanza kuchunguzwa.

Vyanzo vyetu makini kutoka jeshi la polisi zinasema kuwa mali zinazochunguzwa kutokana na tuhuma hizo nzito ni maghorofa, fedha pamoja na magari anayomiliki. “Tuliambiwa kuwa huyu bwana alikuwa akiishi maisha ya hali ya juu, sasa kutokana na tuhumza zake polisi wameanza kuchunguza kila alichonacho ili kujua uhalali wake,” kilisema chanzo.

Chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa, kuna baadhi ya watoto wa vigogo akiwemo mtoto wa meya mmoja wa zamani (jina tunalihifadhi), jijini Dar es Salaam ambaye anadaiwa kuwa alikuwemo katika mkumbo wa kukamatwa Chonji lakini alitoroka na sasa anasakwa na polisi.

Kamanda wa Kikosi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya nchini, SACP Godfrey Nzowa alipotafutwa na gazeti hili ili afafanue madai hayo alisema uchunguzi wa mali za wote wanaotuhumiwa kukamtwa na dawa za kulevya ni lazima ufanyike.

“Tunachunguza mali zao wote waliokamatwa na tuhuma za dawa za kulevya na siyo kwa Chonji peke yake, inapodhihirika kuwa ni za madawa huwa wanafilisiwa,” alisema Kamanda Nzowa. Chonji na wenzake wanne walikamatwa usiku wa manane Oktoba 21, mwaka huu nyumbani kwake Magomeni Mtaa wa Kondoa jijini Dar  na inadaiwa walikuwa  na mzigo wa unga uliokuwa ukifungwa katika vifurushi vidovidogo pia anadaiwa kukutwa na sare za jeshi (JWTZ) na bastola.

Mwimbaji Baby Madaha Adaiwa Kuambukizwa Gonjwa Baya

Posted: 25 Nov 2014 02:57 AM PST

MSANII wa Bongo Fleva, Baby Madaha anadaiwa kuambukizwa gonjwa hatari la zinaa ambalo halikutajwa jina lakini likielezwa kuwa linampa wakati mgumu kisaikolojia. Chanzo kimoja kimeiambia show bize kuwa, nyota huyo amekuwa akitumia dawa za kusafisha haja ndogo kwa muda mrefu lakini bila mafanikio.

Show bize ilimsaka Baby Madaha mwenyewe ambapo aling’aka kwa ukali.
“Hizo habari nani kakupa wewe? Hayo si moja ya maisha ya wanadamu kwani kipi kibaya hapo? Oke, sawa naumwa na hao wanaume wanaotaka nikatibiwe wanajua mimi naumwa nini? Magonjwa ya zinaa si yana dawa?” alihoji.

Hata hivyo, mrembo huyo alisema yeye ana tatizo la haja ndogo kuwa chafu lakini si ugonjwa wa zinaa.

Muhongo Ahusishwa Wizi Nyaraka za Escrow Bungeni

Posted: 25 Nov 2014 02:50 AM PST

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, ametajwa kuwa na uhusiano wa karibu na mmoja kati ya vijana wawili wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kuiba kutoka Ofisi ya Katibu wa Bunge ripoti ya ukaguzi wa hesabu za zaidi ya Sh. bilioni 300 zilizochotwa kifisadi kwenye akaunti ya Tegeta Escrow, iliyoko Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Ukaguzi huo ulifanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).Wakati Waziri Muhongo akitajwa kuwa na uhusiano wa karibu na mtuhumiwa huyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda, ambaye jana ilikuwa ni siku yake ya kwanza kuongoza Bunge tangu lianze Novemba 4, mwaka huu, anadaiwa kutajwa kuwamo katika orodha ya vigogo waliovuna fedha hizo, huku yeye akipata mgawo wa Dola za Marekani milioni moja.

Aliyemtaja Waziri Muhongo kuwa na uhusiano wa karibu na kijana huyo, ni Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika.

Mnyika alimtaja Waziri Muhongo, wakati akichangia mjadala kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2014, bungeni jana.

Muswada huo uliwasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, bungeni, Ijumaa wiki iliyopita.

”Mheshimiwa Spika, ni muhimu ofisi yako ifuatilie. Kwa sababu mtuhumiwa yule ana uhusiano wa karibu sana na Prof. Sospeter Muhongo, ambaye ni mmoja wa watuhumiwa kwenye kashfa tunazozijadili,” alisema Mnyika.

Aliongeza: “Sasa nasema haya mapema ili isifikie hatua tukatumiwa kisingizio cha mambo kuwa mahakamani kushindwa kuwataja kwa majina wahusika. Polisi wafanye uchunguzi, wachukue hatua.”

Mnyika alisema uharamia kwenye suala IPTL wa muda mrefu umezidi mipaka.

Alisema taarifa alizonazo ni kwamba, polisi wanamshauri Spika wa Bunge kwa sababu wanataka haraka haraka wamkimbize mtuhumiwa huyo mahakamani ili baada ya hapo alieleze Bunge kuwa kishapelekwa mahakamani, hivyo hakuna sababu ya kutaja jina wala suala lake kujadiliwa.

Mnyika alisema tangu siku waliyowapa polisi taarifa, mpaka leo wamekuwa wakisitasita wakishindwa kutaja jina la mtuhumiwa, huku wakisingizia uchunguzi.
Hata hivyo, alisema upande wa serikali wanapokutana nao kwenye korido wamekuwa wakiwaambia kuwa mhusika anafahamika, ikiwa ni pamoja na watu wote ambao amekuwa akiwasiliana nao.

“Mheshimiwa Spika, ukiendelea kuyakinga mambo haya kwa kisingizio cha mambo kuwa polisi, halafu baadaye polisi wakaenda mahakamani, ukaja kuyakinga hapa kwa kisingizio cha kwamba mambo yako mahakamani, maana yake Mheshimiwa Spika na wewe utahesabika kwamba, hizo mbinu za hao maharamia waliopora ripoti ndani ya ofisi yako pengine na ofisi yako inahusika,” alisema Mnyika.

Udaku Specially

unread,
Nov 26, 2014, 4:43:00 PM11/26/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Nani Anafaa Kuchukua Mikoba ya Pinda

Posted: 26 Nov 2014 09:21 AM PST

Kwa kazi nzuri na uzalendo walio onyesha ndugu Filikunjombe na Zitto ingekuwa busara Filikunjombe apewe mikoba ya Pinda maana najua magamba hawawezi kumpa Zitto

Lakini kwasababu serikali hii wanapeana kimasirahi basi atapewa mzembe mwingine

Naomba pia tutambue juhudi za Kafulila katika ushindi wa leo kwani bila yeye huu uozo ungepita kimya kimya..kwenye kweli uongo hujitenga. Mkono wa Mungu upo juu ya taifa letu,safari Hii Hawa watu waburuzwe mahakamani

Sababu ya Report ya Tegeta ESCROW Kuwasilisha Bila Pingamizi

Posted: 26 Nov 2014 09:19 AM PST

Nadhani ni lazima iwasilishwe hili tupate misaada iliyofungwa. Na sio kumtafuta mchawi au kutatua tatizo, bali lengo nadhani ni kupata kitumbua kilicho sitishwa. 

Ulaya watapata taarifa ya kinachojiri na watatoa kitumbua, ili tupate ngawira za madawa au afya, elimu, .....

Ebu fikiria, jana na leo Tanga hospital wanatumia plastics badala ya gloves kutoa huduma ya kujifungua au ukunga. Bila misaada nchi haiendi. 

Unapotembea juu ya yanayojiri, angalia mbali na sio chini au unachokiona karibu. 

Chambua mwenyewe ujiridhishe. Au mnasemaje. Changia, kwanini ripoti imekubalika kusomwa.

Hizi ni Tabia Sugu za Wanaume wa Kibongo

Posted: 26 Nov 2014 08:17 AM PST

TABIA SUGU ZA WANAUME WA KIBONGO
1. Ukali
2. Ulevi
3. Kuchelewa kurudi nyumbani
4. Kupenda marafiki kuliko familia
5. Umalaya
6. Kuficha mambo yao ya maendeleo
7. Kupenda hawara kuliko mke
8. Ubabe
9. Ubishi
10. Kusafiri bila kuaga wake zao zaidi huaga nyumba ndogo
11. Uchoyo
12. Bajeti kali nyumbani kwenye bar na nyumba ndogo ipo juu
13. Kusaidia watu baki kuliko ndugu zao
14. Kosa dogo ndani ya nyumba kelele nyingi
15. Hupenda kutoa sana ofa bar hasa akiwa na demu
16. Anapenda kuchapa nje ila akichapiwa mtajua watu wote
17. Akikusaidia mshikaji lazima akutangaze
18. hapendi kutoka na mkewe kwenye party
19. Simu yake ina nywila nyingi sana
20. Simu yake hataki iguswe lakini yeye aguse ya mkewe

Leo Ndio Leo Waliokula Fedha Escow Wanaendelea Kutajwa Laivu Bungeni Muda Huu

Posted: 26 Nov 2014 07:56 AM PST


Leo Ndio Leo Waliokula Fedha Escow Wanaendelea Kutajwa Laivu Bungeni Muda Huu , Baada ya jitihada mbali mbali kufanywa ili Report ya Uwizi wa Fedha za IPTL isiweze Kusomwa Bungeni ..Ila mpaka navyoongea muda huu Report inaendelea kusomwa na Waliokula Fedha wanaendelea kuwekwa Hadharani ...
Stay Tuned....Tutarudi Baadae

Sakata la wizi wa Mabilioni ya Escrow, Mkono, 'Licha ya kulishwa sumu sitohama Tanzania'

Posted: 26 Nov 2014 07:47 AM PST

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), amesema licha ya kulishwa sumu na watu asiowajua hatohama Tanzania kama anavyoshauriwa.

Mkono, pia amegoma kuzungumzia sakata la IPTL na akaunti ya Escrow hadi apate kibali cha Mwanasheria Mkuu, Jaji Frederick Werema.

Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari juu ya tukio la kulishwa sumu na kulazwa hospitalini nchini Uingereza.

Mkono, alisema Novemba 11 mwaka huu akiwa na wabunge wenzake wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, walikwenda nchini Uingereza kwa ziara ya kikazi, ambako alipofika huko aliugua ghafla na kukimbizwa hospitali.

Alisema akiwa hospitali, wabunge wenzake wakiongozwa na Mwenyekiti William Ngeleja, waliwasiliana na ndugu zake juu ya tukio hilo na waliwapa maelekezo ya kuwasiliana na daktari wake (Mkono), Dk. Kapteni

Mkono, alisema Dk. Kapteni anayefanya kazi hospitali ya TMJ, aliwaelekeza wenzake dawa za kumpa kwa kuwa alihisi amelishwa sumu.

“Ukweli nimelishwa sumu, madaktari wameshathibitisha jambo hilo…sijui kina nani walionifanyia hivi, uchunguzi wa aina ya sumu na mtu aliyenipa bado vinaendelea…, waliotenda hivi wanajidanganya,” alisema.

Mkono, alisema akiwa jijini Dar es Salaam alitumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms), ikimtahadharisha juu ya safari yake na madhara atakayoyapata.

Alisema baada ya kutumiwa ujumbe huo, aliwaonyesha wenzake ambao walimtia moyo na kumtaka awe muangalifu na nyendo zake.

Mkono, alisema ujumbe huo utakuwa ni sehemu ya uchunguzi wa tukio lake aliloliita ni la kihuni, lilifanywa na wahuni wasiomtisha.

“Nimeshauriwa nihame Tanzania kwa kuwa tumefikia hatua mbaya, lakini mimi nimesema sihami kwa sababu ya wahuni wachache,” alisema.

Alibainisha kulishwa sumu kwa wabunge si jambo geni hapa nchini, kwa kuwa hata Waziri wa Uchukuzi Dk. Harisson Mwakyembe, alifanyiwa hivyo na kukimbizwa nje ya nchi kwa matibabu.

Kuhusu IPTL

Hata hivyo, Mkono hakuwa tayari kuzungumzia tukio la kulishwa sumu na sakata la IPTL linaloendelea bungeni, ingawa alisema kuna watu anawahisi kuhusika.

Alisema kuwa, alianza kushiriki kesi za IPTL mwaka 1997 akiliwakilisha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), na kila kitu kilifanyika kwa uwazi na kipo kwenye mitandao.

Mkono, alisema hawezi kuzungumzia masuala ya IPTL bila kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa sababu kazi aliyoifanya alipewa na serikali.

Alisema kwa mujibu wa maadili ya uwakili, hapaswi kutoa siri au jambo lolote la mteja wake bila kibali kutoka kwa mhusika.

Polisi wagoma

Jana, Tanzania Daima lilipata habari kwamba polisi walimuhoji Mkono juu ya madai ya kulishwa sumu.

Gazeti hili liliwasiliana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi (SSP), Advera Senso, ili kufahamu kuhusu mahojiano hayo, ambako hakuwa tayari kuweka wazi na aliomba kupewa taarifa zaidi askari waliomuhoji Mkono walitokea wapi.

“Ni vyema ukajiridhisha kwanza kama hao askari wanatokea hapa kwetu au wanatoka kanda maalum …maana inaweza kuwa askari hao wanatimiza wajibu wao wa kawaida wa majukumu ya kazi hivyo jiridhishe halafu unipigie tena,” alisema.

Tanzania Daima halikuishia hapo, liliwasiliana na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna (CP), Suleiman Kova, ambaye alitaka kujua eneo alilopewa sumu hiyo.

“Naomba unieleze mahali au eneo alilonyweshwa sumu ili nijaribu kufuatilia au ameiripoti wapi hiyo taarifa maana sasa sina taarifa,” alisema.

Tanzania Daima

Polisi Ang'olewa Meno Sita na Wananchi Huko Shinyanga

Posted: 26 Nov 2014 05:18 AM PST

Kumetokea tukio la aina yake katika mgodi wa madini ya almasi wa Mwaduiuliopo katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ambapo askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga Pc Idd Makame(25) amejeruhiwa vibaya mdomoni kwa kung’olewa meno sita baada ya kupigwa jiwe kwa kutumia kombeo (kwa lugha ya kisukuma Nh'ago) na watu wanaodaiwa kuwa ni wachimbaji haramu wa madini katika mgodi wa Mwadui wakati akitimiza wajibu wake wa kuhakikisha usalama wa raia na mali zao.

Tukio hilo limetokea Novemba 21,2014saa mb ili na robo usiku katika eneo la Tanex katika mgodi huo wakati askari huyo akiwa na askari wenzake wakiongeza nguvu baada ya askari wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth inayolinda mgodi wa Mwadui kushindwa kuwadhibiti wachimbaji wadogo wa madini maarufu "Wabeshi" waliotaka kuingia kwa nguvu mgodini wakiwa na silaha za jadi. 

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited inayolinda mgodi huo ilipata taarifa kuwa kuna wachimbaji haramu maarufu kwa jina la Wabeshi walitaka kuvamia mgodi wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mishale, mikuki, virungu, makombeo, mapanga.

na fimbo. Kufuatia hali hiyo askari hao wa Zenneth walifika eneo la tukio kuwadhibiti Wabeshi hao lakini ghafla walianza kushambuliwa kwa silaha za jadi yakiwemo marungu, mishale, mikuki na makombeo. Baada ya kuona wanazidiwa nguvu,askari wa Zenneth walilazimika kuomba msaada wa askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) cha jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga. 

Baada ya askari wa FFU kufika eneo la tukio nao walianza kushambuliwa na Wabeshi hao ,ndipo PC Idd akapigwa jiwe mdomoni kwa kutumia kombeo na kung’oka meno sita mdomoni na kukimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited Elisha Ndulu amethibitisha uwepo wa tukio hilo. 

Naye mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Mfaume Salum amesema Pc Idd alipigwa na kitu chenye ubapa mdomoni na kusababisha meno sita kung’oka na anaendelea kupatiwa matibabu,hali yake inaendelea vizuri. Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari wanawashikilia watu wanne kwa mahojiano zaidi na wanaendelea kufanya uchunguzi.

Mahakama ilimshindwa Davido, inawezaje kuzuia Escrow Bungeni?

Posted: 26 Nov 2014 05:08 AM PST

Oktoba 18, mwaka huu, mwanamuziki kutoka Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’ alipanda jukwaani, akatumbuiza na kuondoka kurudi nchini kwao bila kupata usumbufu wowote.

Davido alipanda jukwaa la Fiesta wakati kulikuwa na Amri ya Zuio kutoka Mahakama ya Kisutu, ikiikataza Kampuni ya Prime Time Promotion kumtumia Davido kwenye shoo ya Fiesta kutokana na mgogoro wa kimkataba baina yake na Kampuni ya Times Promotions and Entertainment, vilevile alinyimwa kibali na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

Hata hivyo, Davido alipanda jukwaani na hakuna uamuzi wowote wa dharura ambao ulichukuliwa kutoa fundisho kwa wakaidi wa Amri ya Zuio. Ile adhabu ya kudharau mahakama (Contempt) haikufanya kitu.

Ni aibu kubwa kwa taifa letu ambalo linaongozwa na misingi ya sheria na dola. Ni nchi isiyokuwa na dola peke yake ndiyo alichokifanya Davido hapa nchini kinaweza kutokea na kuvumiliwa kana kwamba hakikutokea kitu. Mahakama haikuona aibu hii!

Kama kwa Davido ilitokea hivyo, nitashangaa sana kama bunge litanywea na kuamua kusitisha hoja nzito yenye maslahi mapana kwa taifa. Bunge linaweza kuendelea na kazi yake. Halafu wahusika waendelee kutapatapa mahakamani. Swali; kama kweli ni watu wazuri na walitenda kilicho halali na haki, wasiwasi wa kukimbilia mahakamani wa nini wakati Ripoti ya Escrow haijasomwa?

Jibu ni kwamba wanajua walichokifanya na wanaelewa kilichomo ndani ya Ripoti ya Escrow na wanatambua nini ambacho kinaenda kusomwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, kwa maana hiyo ni waelewa wa kile kinachokaribia kuwapata. Ripoti isomwe, hata wakizuia itavuja na wananchi watachukua uamuzi. Tuache kulinda ufisadi kwa amani yetu na maendeleo ya uchumi wetu.

Mungu ibariki Tanzania.

Aliyekuwa Mke wa Muheshimiwa Sugu Afyatua Matusi Mtandaoni

Posted: 26 Nov 2014 05:04 AM PST

Mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, mwanadada Faiza Ally ameamua kuwatolea uvivu watu wanaodai kuwa ameachwa na mheshimiwa huyo kutokana na mavazi yake. 

Faiza ambae ana mtoto na Sugu, katika instagram ameandika:
“Sasa leo ngoja nifunguke…. Yaani nikiweka picha zangu kwa raha zangu mnaanza kusema oh ndio maana SUGU kakimbia ndio maana kaniacha Nasema hivi MIMI NDIO NIMEMUACHA mkome kunisema nimeachana na nimemuacha tukiwa kwenye process za ndoa na tulishakutana na padri na kwenye jumuiya nilisha anza ….. 

Kuna vitu vikinifanya niondoke kabla ya ndoa ambavyo vitabaki kuwa vya kifamilia ……. Nyie mna muona sugu Kama si mtu wa kawaida mm namuona Kama alie kuwa mpenzi wangu na Sasa ni baba wa mtoto wangu …. Lkn anajua ubora wangu na faida zangu Pumbavu zenu nyote mnao zani niliachwa tena kwa mavazi anajua na anapenda mavazi yangu ….. Nachukia kuamka asubuhi na kukuta comments za kusemwa vibaya…. Nyie mnajua tabia zake ????? Au mnamuona kwa mbali ?????”

Wema Gives a Comment on Zari and Diamond's K!ssing Photo

Posted: 25 Nov 2014 08:49 PM PST

Kumekucha ...Wema Gives a Comment on Zari and Diamond's K!ssing Photo...

DK Cheni Alishwa Sumu Tena..Kunani?

Posted: 25 Nov 2014 08:27 PM PST

Stori: Imelda Mtema
Staa wa kiume wa sinema za Kibongo, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’, kwa mara nyingine alilazwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar baada ya kudaiwa kula chakula kinachosadikika kuwa na sumu (poisonous food).

Akizungumza na mwandishi wetu wikiendi iliyopita Dk Cheni alisema kuwa alikuwa mshehereshaji (MC) kwenye harusi moja iliyofanyika maeneo ya Sinza jijini Dar ndipo akala chakula hicho ambapo muda mfupi baadaye alianza kujisikia vibaya ‘kichina’.

Staa huyo alisema kuwa baada ya hatua chache kutoka ukumbini, tumbo lilianza kumuuma kisha akaishiwa nguvu ndipo akaweka gari pembeni na kupiga simu kwa ndugu kuomba msaada.
Dk Cheni aliendelea kueleza kuwa baada ya kupata msaada moja kwa moja alipelekwa kwenye Hospitali ya Burhani jijini Dar.


Alisema kuwa baadaye alihamishiwa kwenye Hospitali ya TMJ ambapo madaktari walipompima waligundua alikuwa amekula chakula chenye sumu ndipo wakampatia matibabu na kulazwa.
Alisema siku ya pili yake aliruhusiwa huku akisema kitendo hicho kimemsikitisha mno.

Siyo mara ya kwanza kwa Dk Cheni kulishwa chakula chenye sumu kwani safari hii ni mara ya pili ambapo mwaka jana alilazwa tena kwa ishu kama hiyo, jambo ambalo haelewi kwa nini inakuwa hivyo.
GPL

Udaku Specially

unread,
Nov 27, 2014, 4:45:29 PM11/27/14
to mbara...@googlegroups.com

Udaku Specially


Mahakama Kuu Yamwachia Huru Sheikh Ponda Leo

Posted: 27 Nov 2014 08:29 AM PST

MAHAKAMA  Kuu ya Tanzania imemuachia huru aliyekuwa Katibu wa Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda baada ya kuona hana hatia dhidi ya Kesi ya madai ya Ardhi ya Agrekanza inayomilikiwa na Afidhi Self  iliyokuwa inamkabili.

Akisoma Mashtaka hayo Mwanasheria wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Jaji, Augustino Shangwe alisema baada ya kupitia vifungu vyote mahakama imejiridhisha na kuona Sheikh Ponda hana hatia yoyote na kumuachia huru tangu leo lakini katika hali ya kushangaza Sheikh Ponda amerudishwa rumande akisubiri kesi nyingine ya madai ya uchochezi,  Mkoani Morogoro inayomkabili.

ESCROW:Majibu ya PROF MUHONGO ni Aibu ya Mwaka kwa PAC na Wasaka Tonge

Posted: 27 Nov 2014 07:35 AM PST

Kwa aliyefatilia majibu ya waziri wa nishati na madini profesa Sospeter Muhongo leo bungeni akijibu hoja za kamati ya PAC atakubali kuwa kamati ya ZITTO KABWE imewadanganya watanzania. Muhongo ambaye amejibu hoja moja baada ya nyingine kwa kutoa ushahidi wa viambatanisho muhimu amedhihirishia bunge kuwa kamati ya bunge imetoa taarifa ya uongo. 

Katika majibu yake, profesa Muhongo amedhihirisha kwa ushahidi kuwa pesa za ESCROW hazikua za serikali. Pesa hizo ni za IPTL na kwamba serikali bado inadaiwa kiasi cha shilingi bilioni 94 na IPTL kama malipo ya kufua umeme. 
Aidha, Muhongo amemlipua mwanasheria Mkono ambaye aliingia mkataba na TANESCO wa kuwa mwanasheria wao na alidai na kulipwa kiasi cha bilioni 62 (robo ya pesa za ESCROW) kama malipo ya uanasheria. Mkataba huu ulivunjwa na TANESCO chini ya uongozi wa waziri Muhongo. 

Majibu haya ya Muhongo yameivua nguo kamati ya PAC na kuzua maswali mengi yasiyo na majibu. 
Kwanini PAC ilidanganya bunge? 
Kwanini PAC haikuonesha vielelezo hivyo? 
Nani yako nyuma ya PAC? 
Kwanini PAC haikutaja ufisadi huu wa Mkono? 
Taarifa kuwa wasaka Urais wa CCM ndio waliopika uongo huu tuziamini? 

Asali Asili (Nature Honey) Inapatikana Kwa Bei Poa Kabisa

Posted: 27 Nov 2014 03:35 AM PST



Ngase Company Limited Inakuletea Asali Asili Kabisa ikiwa imepakiwa Kwenye Chupa kwa usafi wa hali ya juu, 

PACKAGES & PRICE
Carton of 12 Jars of 500g Each, Price is 96000/= Per Carton

Wanapatikana Tegeta Wazo Hill
Wasiliana Nao Kwa Number zifuatazo:

TEL: 0737 209890
MOB:0756669494
0655418466
0777418466

E –mail: sa...@ngasecompanyltd.com
ngamanya.k...@ngasecompanyltd.com



Mwanamke ni Kiumbe katili Kuliko Hata Unavyofikiria

Posted: 27 Nov 2014 03:04 AM PST

Mara nyingi sana watu wamekuwa wakiwasifu wanawake kwamba ni watu wapole lakini ukweli haupo hivyo.

Mwanamke ni mtu wa maamuzi ya haraka na pengine anapotaka kufanya jambo huwa hafikiri madhara yake huwa anakuja kutafakari wakati nambo yamesha haribika.

Mwanamke akiwa na hasira anakutoa roho muda wowote na anabadilika tabia muda wowote. Ukitaka kuamini embu siku moja muulize mkeo kwamba hivi nikizaa nje mtoto upo tayari kuishi naye halafu usikie majibu atakayokupa. Niliwahi kumueleza mke wangu nataka kuoa mke wa pili jibu alilonipa kwamba nisimtafutie mada kesi tafadhari , jibu ambalo mpaka leo huwa najiuliza alikusudia nini.

Mwanamke si mtu wa kumsaidia kwa sababu hawana shukrani na wepesi mno kusahau fadhira walizo tendewa. Unaweza kuwa na mke ukampa kila kitu lakini siku moja akimpata wa nje utapata tabu.

Wanawake ni wepesi sana kudanganyika hata asome vipi ni wachache mno unao weza kuwakuta na misimamo imara.


Au siku moja partner wako akiwa na mimba jaribu kumwambia mimba hii nina mashaka si yangu halafu uone response ya kikatili utakakuta katoto kenyewe kametupwa jalalani huko .

The Nyama Choma Festival Dar 6 Desemba – Jipatie tiketi yako kwa shilingi 7,000 tu

Posted: 27 Nov 2014 02:24 AM PST

Tembelea vituo vya mauzo ujipatie tiketi yako Sasa.

1.Samaki Samaki-Mlimani City Na Posta

2.Tripple 7 Kawe

3.Didis Oysterbay

4.Born 2 Shine Mwenge

Baada ya ishu ya Escrow, Haya ni Majibu Mawili ya Waziri Mkuu Pinda ikiwemo Kujiuzulu

Posted: 27 Nov 2014 01:27 AM PST

Kikao cha Bunge leo Novemba 27 kimeanza kwa maswali mawili kuulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda
.
“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungen, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“– Mbowe.

Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.

Baada ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, nini msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za watu binafsi na sio fedha za umma?“– Mbowe.
Kwa uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.
Akijibu maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…“

Ningeweza nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Baada ya majibu hayo, Mbowe alipata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Waziri Mkuu; “…Pamoja na kwamba jambo hili litajitokeza baadaye katika mijadala ya leo, bado haiondoi ukweli kwamba una wajibu wa kulijibu swali langu. Naomba kwa heshima sana nikuulize tena kwa mara nyingine, taifa limepata fedheha kubwa sana kutokana na sakata hili, nchi nzima inasikiliza tatizo hili…“– Mbowe.

“…Una heshima kama kiongozi wa Serikali lakini heshima ambayo itakuwa imethibitishwa zaidi kama utaamua kujiwajibisha mwenyewe ili kuweka heshima yako na heshima ya Serikali, je kwa mara nyingine huoni ingekuwa vema kama basi utujibu kama unafikiri bado zile fedha ni za umma kama hutaki ku-declare kujiuzulu katika hatua ya sasa?”– Mbowe.

Nimekurekodia sauti ya wakati maswali hayo yakiulizwa na kujibiwa Bungeni leo Dodoma, unaweza kusikiliza kwa kubonyeza play.

Diamond Platnumz Kuingia Kwenye Jumba la BBA Hotshots leo (Nov 27) Kupiga Story na Washiriki

Posted: 27 Nov 2014 12:49 AM PST

Diamond Platnumz tayari ametua jijini Johannesburg, Afrika Kusini toka jana, tayari kuhudhuria tuzo za Channel O (CHOAMVA) zinazotarajiwa kutolewa siku ya Jumamosi Nov.29 akiwa anawania vipengele vinne.

Staa huyo ambaye ameachia ngoma mpya siku chache zilizopita ‘Ntampata wapi’, ameandika kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamaii kuwa pia leo Alhamisi Nov.27 atapata nafasi ya kuingia kwenye jumba la Big Brother kubadilishana mawazo na washiriki.

“Tafadhali usikose kuangalia Big Brother Afrika kuanzia saa tano Asubuhi kesho (leo), kijana wako Platnumz ntakuwa ndani ya nyumba nikizoza mawili matatu na washiriki….” aliandika Diamond.

Drama: Wema kuhudhuria show ya Chameleone, Diamond kuwa mgeni wa show ya Zari, zote kufanyika siku 1

Posted: 27 Nov 2014 12:43 AM PST

Taarifa zilizosambaa ni kwamba Wema na Diamond wanatarajiwa kwenda Uganda December, lakini kila mmoja akiwa na mwaliko wa mwenyeji tofauti. Diamond atakuwa mgeni kwenye show ya Zari The boss lady, huku Wema atakuwa mgeni wa show ya Jose Chameleone.

Maswali ya uhusiano wa staa wa filamu Wema Sepetu pamoja na staa wa muziki Diamond Platnumz yamezidi kuongezeka kama kweli wameachana ama laa, baada ya wote wawili kujihusisha kupigia debe show hizo mbili tofauti zinazotarajiwa kufanyika siku moja, mwezi mmoja, jiji moja lakini kumbi tofauti.

Diamond ambaye amekana kuwa hana uhusiano wowote wa kimapenzi na Zari, amepigia debe show ya ‘Zari All White Ciroc Party’ huku akitarajiwa kuwa mgeni kwenye show hiyo. Kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii ameandika:

kama mlivyokuwa kimya wakati nasupport watu wengine… Muendelee hivyohivyo…Hasa niwaskie kwenye hii #AllWhiteParty 18th Dec 2014 at Guvnor night club in Kampala UG Usikose!… @zarithebosslady

Huku Wema naye amepigia debe show ya Jose Chameleone ‘1 Man, 1 Show, 1 Million’ huku akiahidi kwenda Uganda kuhudhuria show hiyo, ameandika:

Hatari….!!!! Hatari….!!!! Hatari….!!!!! Sijawahi kufika Uganda lakini kwa hii ntapanda ndege kabisa kwenda kumsupport my brother @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone …. Basi tutakutana pale kati tar 18 kwenye hio show ya kufunga mwaka… Ama nene….”

Show zote mbili ya Zari na ya Chameleone zinatarajiwa kufanyika Kampala siku moja ya Dec.18.

Hakuna Atakayeachia Ngazi Sakata la Escrow

Posted: 26 Nov 2014 09:43 PM PST

Baada ya kusikiliza ripoti rasmi ya PAC iliyowasilishwa na Zitto Kabwe na Deo Filikunjombe nnadiriki kusema kuwa hakuna cha maana kwenye ripoti yao cha kuwafanya mawaziri kuwachia ngazi.

Ni drama tu lakini hakuna kipengele chochote cha sheria ambacho hakijibiki au kilichooneshwa kuwa kimekiukwa.

Hukumu ya Mahakama ni ya halali na haina utata na Zitto wala CAG wala TAKUKURU hawajaonesha kuwa ilikuwa ni batili au ya kughushi. 

Zitto kapiga porojo nyingi sana kuliko ukweli, na mwanasheria yoyote mahiri anazisambaratisha hoja zake zote ndani ya nusu saa.

Zitto ametetea sana BoT lakini alichoshindwa kuelewa ni kuwa Bot kama wakala ndiye alitakiwa aridhike na vielelezo vyote kabla hajalipa na kama havijakamilika hawezi kutoa fedha. Zitto anasema eti Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye alimuamuru Gavana hizo fedha zitolewe, toka lini Gavana wa benki anatoa fedha kwa amri ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali? 

Utata wa IPTL na Standard Chartered ni huko-huko kwao si IPTL iliyokopa, iliyokopa ni Mechmar na Mechmar haiwezi jitokeza kwani imeshafilisika kisheria, Standard Chartered karata yao ya mwisho ni hii na hapa wamepata mwanya.

Nnasikitika kusema na nnaliona linakuja la Serikali kuingia gharama kubwa ya kulipa zaidi ya mara mbili au tatu hizi fedha ikiwa watafata akili za akina Zitto.

Nnashauri, wajadili hili suala bungeni lakini shauri liwachwe kesi kumi zilizopo mahakamani zinazoihusu IPTL zikamilike.

Mapendekezo ya Zitto ya watu kuachia nyadhifa zao ni ya kishabiki na hayana mshiko, watu hawaachii tu nyadhifa zao kwa habari kama hizi ambazo hazina mshiko wa kisheria.

Isitoshe, fedha zilizolipwa escrow si kamili, hizo zilizobaki zilizuiliwa kwanini? Jibu tutalipata kesho na ndilo litakalosambaratisha hoja ya kodi ya Zitto. 

Kuna mengi sana ya kuchambua lakini tusubiri leo, tusiandikie mate na wino upo. Ni matumaini yangu kuwa wote waliotajwa watapewa fursa ya kujibu. Na hapo ndipo mtamjuwa Chenge ni kichwa.

By  FaizaFoxy

Dida Afunguka Kuhusu Ezden Kuoa Mke Mwingine Baada ya Wao Kuachana

Posted: 26 Nov 2014 09:34 PM PST

Na Imelda Mtema
MTANGAZAJI mwenye maneno lukuki kutoka Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amesema kuwa endapo mtalaka wake, Ezden Jumanne akitaka kuoa yeye atakuwa wa kwanza kutoa mchango wa harusi hiyo.

Dida ambaye kwa sasa yupo singo, alisema japokuwa wameacha na Ezden, lakini hana bifu naye kwa sababu anaamini kuwa yuko katika harakati za kutafuta mke bora hivyo haoni shida kumchangia.

“Ninachoamini mimi Ezden bado anasaka mke mwema na hiyo ni nzuri na wala siwezi kuwa na bifu na mtu wake yeyote atakayempata, nitapenda sana. Haya ndiyo maisha yasiyokuwa na chuki yanayotakiwa,” alisema Dida.

Mganga wa Kienyeji Aibuka na Kutoboa Siri Nzito Kuhusu Mwimbaji Meninah

Posted: 26 Nov 2014 09:30 PM PST

Na Stori: Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani
Mganga aliyejita-mbulisha kwa jina moja la Kimweri ameibuka na madai mazito kuwa ndiye aliyemng’arisha staa wa kike wa Bongo Fleva, Meninah Abdukareem ‘Meninah La diva’ hivyo kutoa siri nzito ambayo wengi hawakuijua.Kwa mujibu wa chanzo makini, mganga huyo amekuwa akimfanyia ndumba msanii huyo ili arudiane na aliyekuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinum’.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mganga huyo amekuwa akidai kwamba, huwa msanii huyo anatinga nyumbani kwake maeneo ya Mwananyamala-Komakoma jijini Dar kisha kumlilia shida yake akimtaka afanye juu chini kuhakikisha anamrudisha Diamond mikononi mwake.

Baada ya kukisikia chanzo hicho, waandishi wetu walikwenda nyumbani kwa mganga huyo na walipomuuliza ishu hiyo alikiri Meninah kufika kwake ili kufanyiwa ndumba arudiane na Diamond.

“Yule msanii anayeitwa Meninah ambaye habari zilivuma kuwa anatoka na Diamond na kukanusha, huwa anakuja hapa kufuata tiba na kikubwa anachokitaka anataka nimvute Diamond ili warudiane,” alisema.
Meninah alipoulizwa kuhusu madai hayo aliruka kimanga na kudai hakuwahi kuwa na uhusiano na Diamond na wala hamjui mganga huyo.

“Yule msanii anayeitwa Meninah ambaye habari zilivuma kuwa anatoka na Diamond na kukanusha, huwa anakuja hapa kufuata tiba na kikubwa anachokitaka anataka nimvute Diamond ili warudiane,” alisema.
Meninah alipoulizwa kuhusu madai hayo aliruka kimanga na kudai hakuwahi kuwa na uhusiano na Diamond na wala hamjui mganga huyo.

Sendeka Asema Tutauana Lakini Pinda Hajiuzulu Katu

Posted: 26 Nov 2014 09:27 PM PST

SENDEKA asema tutauana lakini PINDA hajiuzulu katu. 
Kikao cha wabunge wa CCM kinachiendelea mchana huu kimekuwa moto mbali. Christopher Ole Sendeka mbunge wa Simanjiro amesema wako radhi kuchinjana bungeni lakini si Pinda kujiuzulu. "Ajiuzulu amekosa nini, ripoti zote hazimtaji popote kuhusika. Kama tatizo ni nia yake ya u Rais, kwani Pinda hana haki ya kugombea? Nasema niko radhi tuchinjane bungeni lakini si kuona mtu anasulubiwa kwa maslahi ya wabinafsi wachache wenye malengo yao ya kisiasa. Kwa hili nitasimama kidete. .."alisema Sendeka huku ukumbi wote ukiwa kimya

Muonekano wa Yule Msichana wa Kazi Aliye Taka Kumuua Mtoto wa Boss Wake Baada ya Yeye Kuchezea Kichapo

Posted: 26 Nov 2014 09:17 PM PST

Huu ndio muonekano wa yule msichana wa kazi za ndani aliye tenda unyama wa kutaka kumuua mtoto wa bosi wake atimaye naye amepokea kipigo takatifu cha nusu kufa kutoka kwa wazazi wa uyo mtoto hii ni moja ya picha zilizo vuja ambazo wazazi wa mtoto family iyo walizificha.

Unaambiwa haya yote yasingejulikana kama Polisi isingemkamata baba mzazi wa mtoto huyu, yani baba alipoona ile video ndioakampiga Msichana huyu wa kazi ambae baada ya kipigo alikwenda kumshitaki baba wa mtoto Polisi.
Polisi walipomchukua Erick Kamanzi (Baba wa mtoto) nyumbani kwa ke na kumfikisha Polisi ambako alieleza sababu za kumpiga Msichana huyu na kuwaonyesha Polisi  video ambayo ni ya tukio la mtoto wake kupigwa.
Baada ya hapo Polisi ndio wakamwachia na kumkamata Msichana 
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages